logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mama wa kambo wa Malala agura Kenya Kwanza, awaidhinisha Raila na Barasa

Okanya anawania kiti cha ubunge cha Mumias Magharibi

image
na Radio Jambo

Yanayojiri03 August 2022 - 17:23

Muhtasari


  • Akizungumza wakati wa mkutano huo, Raila aliahidi kufufua shughuli za Kampuni ya Sukari ya Mumias

Mamake wa kambo wa Seneta wa Kaunti ya Kakamega Cleophas Malala amgura Kenya Kwanza kwa Azimio.

Jackeline Okanya alitangaza kuunga mkono ombi la Raila Odinga wakati wa mkutano wa Azimio katika uwanja wa Bukhungu siku ya Jumatano.

"Nimetoka Kenya Kanza. Nimekuja Azimio kusaidia Baba na Martha. Nimekuja kusaidia gavana wangu Barasa na Savula ili Kenya yetu iweze kwenda mbele,"Alizungumza Okanya.

Okanya anawania kiti cha ubunge cha Mumias Magharibi, ambapo alimhakikishia Raila kwamba eneo hilo litaongozwa na viongozi washirika wa Azimio.

Anagombea kwa tiketi ya ANC. Mnamo Juni 19, aliombwa kuachia ngazi kwa ajili ya Rashid Echesa wa UDA, jambo ambalo alilikanusha.

Barasa wa ODM anawania kiti cha ugavana dhidi ya Malala ambaye anawania kwa tiketi ya ANC, Cyrus Jirongo (UDP), na Samuel Omukoko wa Maendeleo Democratic Party (MDP) miongoni mwa wengine.

Akizungumza wakati wa mkutano huo, Raila aliahidi kufufua shughuli za Kampuni ya Sukari ya Mumias.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved