In Summary

• Ruto atafanya mkutano wake katika uwanja wa Nyayo huku Raila akiwa uwanja wa Kasarani.

Wafuasi wa Naibu Rais William Ruto katika uwanja wa Nyayo mnamo Agosti 6, 2022 Picha: WILFRED NYANGERESI
Image: The Star//WILFRED NYANGERESI

Baada ya miezi kadhaa ya kampeni za kutupiana maneno na cheche kali miongoni mwa wanasiasa, hatimaye kipindi hicho kinafikia kikomo leo kulingana na sheria za katiba kwamba kampeni zitamatishwe angalau siku mbili kabla ya uchaguzi mkuu.

Miungano miwili hasimu Azimio la Umoja One Kenya na Kenya Kwanza imejiandaa vilivyo kuweka rekodi katika siku hii ya mwisho huku mirengo yote ikikongamana katika sehemu tofauti jijini Nairobi.

Azimio wamejumuika katika uwanja wa Kasarani weney uwezo wa kusheheni takribani watu elfu sitini huku Mrengo wa Kenya Kwanza ukiongozwa na DP Ruto ukikongamana uwanja wa Nyayo unaosheheni watu elfu 35.

Awali kulikuwepo na wasiwasi kuhusu uwezekano wa Ruto na Kenya Kwanza kupewa kibali cha kukongamana Nyayo ila Alhamisi mahakama ilitoa amri kwamba waruhusiwe kujumuika pale.

Hapa tunakuandalia baadhi ya picha za kufana kuonesha jinsi wafuasi wa Kenya Kwanza wamejitoma kwenye uwanja wa Nyayo.

Wafuasi wa Naibu Rais William Ruto katika uwanja wa Nyayo mnamo Agosti 6, 2022 Picha: WILFRED NYANGERESI
Wafuasi wa Naibu Rais William Ruto katika uwanja wa Nyayo mnamo Agosti 6, 2022 Picha: WILFRED NYANGERESI
Wafuasi wa Naibu Rais William Ruto katika uwanja wa Nyayo mnamo Agosti 6, 2022 Picha: WILFRED NYANGERESI
Wafuasi wa Naibu Rais William Ruto katika uwanja wa Nyayo mnamo Agosti 6, 2022 Picha: WILFRED NYANGERESI
Wafuasi wa Naibu Rais William Ruto katika uwanja wa Nyayo mnamo Agosti 6, 2022 Picha: WILFRED NYANGERESI
Wafuasi wa Naibu Rais William Ruto katika uwanja wa Nyayo mnamo Agosti 6, 2022 Picha: WILFRED NYANGERESI
Wafuasi wa Naibu Rais William Ruto katika uwanja wa Nyayo mnamo Agosti 6, 2022 Picha: WILFRED NYANGERESI
Wafuasi wa Naibu Rais William Ruto katika uwanja wa Nyayo mnamo Agosti 6, 2022 Picha: WILFRED NYANGERESI
Wafuasi wa Naibu Rais William Ruto katika uwanja wa Nyayo mnamo Agosti 6, 2022 Picha: WILFRED NYANGERESI
View Comments