logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chris Wamalwa akubali kushindwa na Natembeya katika kinyang'anyiro cha ugavana Trans Nzoia

Wamalwa pia alimpongeza Natembeya kwa kutwaa ushindi.

image
na Radio Jambo

Makala11 August 2022 - 18:53

Muhtasari


•Wamalwa pia alimpongeza mgombeaji wa DAP-K George Natembeya akisema ameshinda kinyang'anyiro hicho.

Mgombea ugavana wa Trans Nzoia kwa tiketi ya Ford Kenya Chris Wamalwa amekubali kushindwa.

Katika taarifa aliyochapisha Twitter, Wamalwa aliwashukuru wapiga kura wa Trans Nzoia na chama chake kwa uungwaji mkono waliompa katika kipindi chote cha kampeni.

Mbunge huyo wa zamani wa Kiminini pia alimpongeza mgombeaji wa DAP-K George Natembeya akisema ameshinda kinyang'anyiro hicho.

"Namtakia heri," Wamalwa alisema.

"Sijafaulu katika azma yangu ya kuwa Gavana wa pili wa Kaunti yetu kuu. Namshukuru Mwenyezi Mungu, wafuasi wangu wote kutoka mbali na karibu, kwa usaidizi wao usio na kikomo. Pokeeni shukrani zangu za milele," aliongeza.

Mbunge huyo anayeondoka pia aliwashukuru wananchi wa jimbo la Kiminini kwa kumchagua kuwa mbunge kwa vipindi viwili mfululizo.

"Shukrani zangu za dhati kwa wafuasi wa chama na watu wa kujitolea ambao wamefanya kazi kubwa katika kampeni hii," alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved