In Summary

•Mbunge anayeondoka wa Kajiado Kusini Katoo ole Metito (UDA) aliibuka wa pili kwa kura 111,725 huku gavana wa zamani David Nkedianye (Jubilee) akipata kura 75,337.

•Samuel Seki (UDA) alishinda useneta kwa kura 125,696 mbele ya Judith Pareno (ODM) aliyepata kura 99,943 naye Moses Sakuda wa Jubilee akipata kura 56,380.

Gavana mteule wa Kajiado Joseph Lenku akipokea cheti chake cha uchaguzi kutoka kwa Festus Muchege wa IEBC Jumamosi asubuhi.
Image: KURGAT MARINDANY

IEBC Jumamosi ilimtangaza Joseph Lenku Kajiado wa ODM kuwa gavana mteule kaunti ya Kajiado baada ya kupata kura 117,600 katika uchaguzi wa Jumanne.

Mbunge anayeondoka wa Kajiado Kusini Katoo ole Metito (UDA) aliibuka wa pili kwa kura 111,725 huku gavana wa zamani David Nkedianye (Jubilee) akipata kura 75,337.

Ambrose Kago (mgombea huru) alifuata kwa kura 2,661 katika kiti hicho kilichokuwa na ushindani mkali.

Hata hivyo, madai ya wizi mkubwa yamezingira ushindi wa Lenku huku Metito na Nkedianye wakikataa kukubali.

Katika hotuba yake ya kukubalika, Lenku aliwashukuru wote waliochangia ushindi wake.

"Pokeen baraka tele kutoka kwa Bwana wetu mwema na msikose kamwe kwa kujitolea kwenu kuhakikisha Kajiado inaendelea kuwa na uongozi mzuri," Lenku alisema.

Lenku aliwaambia washindani wake kwamba kutakuwa na nafasi nyingine kwao kushinda.

Katika kinyang’anyiro cha useneta, Samuel Seki (UDA) alipata kura 125,696 mbele ya Judith Pareno (ODM) aliyepata kura 99,943 naye Moses Sakuda wa Jubilee akipata kura 56,380.

Gideon Toimasi (Wiper) alipata kura 8,821 mbele ya Sonia Gitau (Usawa) aliyepokea 8,267 naye Simon Nkeri (TSP) alipokea 7,474.

Leah Sankaire (UDA) alitangazwa mshindi katika kinyang'anyiro cha uwakilishi wa wanawake kwa kura 122,764 mbele ya Jenifer Moinkett wa Jubilee (87,312).

View Comments