In Summary

•Ruto amesema kuwa atatumikia Wakenya kwa usawa kama rais mara tu atakapochukua hatamu kutoka kwa serikali ya sasa.

•"Serikali yetu itatoka nje ya njia yetu na kufanya kazi saa nzima kuhakikisha hilo linafanyika."

Ruto alisema tofauti zilizotokea wakati kampeni sasa ni maji chini ya daraja
Image: ANDREW KASUKU

Rais mteule William Ruto amesema kuwa atatumikia Wakenya kwa usawa kama rais mara tu atakapochukua hatamu kutoka kwa serikali ya sasa.

Akizungumza muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi katika ukumbi wa Bomas of Kenya, Ruto alisema tofauti zilizotokea wakati wa kampeni sasa ni maji chini ya daraja.

Aliahidi kujenga nchi iliyoungana kwa matumaini ya kufanya maisha ya Wakenya kuwa bora.

“Nitabarikiwa sana kuwa rais wa 5 wa Kenya. Najua majukumu mazito yananingoja lakini Wakenya wanajua mimi ni mchapakazi na nitajitahidi sana kutowaangusha,” akasema.

"Serikali yetu itatoka nje ya njia yetu na kufanya kazi saa nzima kuhakikisha hilo linafanyika."

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ilimtangaza kiongozi huyo wa Kenya Kwanza mwenye umri wa miaka 55 kama rais mteule mnamo Agosti 15, 2022.

Ruto alihitaji asilimia 50 pamoja na moja ya kura zote nchini, na asilimia 25 ya kura katika angalau kaunti 24 ili kutangazwa rais.

Ruto alipata kura 7,176,141 ikiwa ni asilimia 50.49 ya kura za mwisho, huku Raila Odinga wa Azimio aliyeshika nafasi ya pili akipata kura 6,942,930 ikiwa ni asilimia 48.85.

View Comments