In Summary
  • Wakala wa ODM awasilisha hati ya kiapo kuunga mkono dai la Ruto kuhusu 'fomu ghushi'
Naibu rais William Ruto
Image: Facebook//WilliamSamoeiRuto

Wakala wa ODM amewasilisha hati ya kiapo kuunga mkono kesi ya Rais-Mteule William Ruto akidai kwamba mojawapo ya fomu zilizoambatishwa katika kesi ya Azimio ni ghushi.

Eric Atuma anasema alikuwa wakala katika kituo cha kupigia kura cha St. Martin School Kibarage 2 kati ya 7 katika Wadi ya Kitusuru, Eneo Bunge la Westlands Kaunti ya Nairobi.

Atuma anadai kuwa alikuwepo kituoni siku ya uchaguzi mkuu hadi na kujumuisha wakati wa kufunga kura.

"Kama wakala, niliangalia na kuzingatia zoezi la kujumlisha kura katika kituo cha kupigia kura mara tu baada ya kufunga kura," alisema.

Atuma anasema baada ya kukamilisha kujumlisha, mawakala wote katika kituo cha kupigia kura walipewa nakala ya fomu 34A iliyotiwa sahihi na kuwasilisha nakala kwa chama changu mara moja( ODM) kielektroniki.

"Nimeonyeshwa nakala ya fomu 34A ambayo tulipokea kutoka kwa afisa msimamizi katika kituo cha kupigia kura na kwa hakika sio nakala ya kielektroniki ambayo niliwasilisha kwa ODM/Azimio," anadai.

Anashikilia kuwa fomu aliyowasilishwa kwa chama ambacho kimewasilisha kortini ni sawa na ile iliyopakiwa kwenye tovuti ya umma ya IEBC.

“Fomu ya 34 A iliyo kwenye ukurasa wa 121 wa hati ya kiapo ya Arnold Oginga si nakala ya kweli ya fomu iliyotumwa kwa chama wala fomu 34A iliyo katika Tovuti ya IEBC,” anadai.

Atuma anasema kama wakala wa ODM katika kituo husika cha kupigia kura,

"Ningependa kuthibitisha kwamba uwakilishi wa kweli wa fomu 34A ndio nilituma chama na kutoa hapa".

 

 

 

 

View Comments