logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mahakama kutoa uamuzi wa kesi ya uchaguzi wa urais kuanzia saa sita mchana

Mahakama ilitangaza hayo Jumatatu katika notisi iliyotumwa kwa vyombo vya habari.

image
na

Habari05 September 2022 - 06:32

Muhtasari


•Jaji Mkuu Martha Koome mnamo Ijumaa alisitisha rasmi kusikilizwa kwa kesi ya rais kabla ya hukumu ya leo.

•Majaji walitumia wikendi nzima kuandika uamuzi wao kuhusu masuala tisa yaliyowasilishwa mahakamani siku tatu zilizopita katika ombi la kupinga kuchaguliwa kwa Naibu Rais William Ruto kuwa Rais Mteule.

Mahakama ya Upeo itatoa maamuzi yake Jumatatu kuhusu kesi ya rais mwendo wa sa sita, Mahakama imesema. 

Mahakama ilitangaza hayo Jumatatu katika notisi iliyotumwa kwa vyombo vya habari.

Benchi la majaji saba linatarajiwa kutoa hukumu zao wenyewe na kuzisoma katika Mahakama ya Upeo.

Saba hao ni pamoja na; Jaji Mkuu Martha Koome, Philomena Mwilu (Naibu Jaji Mkuu) Njoki Ndung'u, Issac Lenaola, Smokin Wanjala, Mohammed Ibrahim na William Ouko.

Koome mnamo Ijumaa alisitisha rasmi kusikilizwa kwa ombi la rais kabla ya hukumu ya leo. 

Majaji walitumia wikendi nzima kuandika uamuzi wao kuhusu masuala tisa yaliyowasilishwa mahakamani siku tatu zilizopita katika ombi la kupinga kuchaguliwa kwa Naibu Rais William Ruto kuwa Rais Mteule.

 Masuala hayo yaliunda sehemu kubwa ya hoja za mawakili kadhaa waliowakilisha Raila Odinga, Ruto, tume ya IEBC, mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebukati na wahusika wengine katika kesi hiyo.

Mawakili walikuwa na siku tatu za kutoa hoja na ushahidi mbele ya mahakama ya majaji saba kuanzia Jumatano.  

Kesi hiyo ilianza Jumanne kwa kongamano la kabla ya kesi baada ya walalamishi na walalamikiwa kumaliza kuwasilisha hati zao za kiapo kufikia Jumatatu. 

Mnamo Ijumaa majaji hao waliwaomba Wakenya kuwaombea wawe na utambuzi wanapoandika hukumu hiyo. 

Mwaka wa 2017 mahakama hiyo iliweka historia kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kubatilisha uchaguzi wa rais.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved