logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Ilifika wakati singeweza kunyonyesha,' Carrol Sonnie afunguka jinsi alivyopambana na msongo wa mawazo

Amekiri kuwa matukio yaliyofuata baada ya kutangaza kutengana kwake na Mulamwah yalimuathiri vibaya

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 February 2022 - 10:15

Muhtasari


•Muthoni alikiri kuwa matukio yaliyofuata baada ya kutangaza kutengana kwake na Mulamwah yalimuathiri vibaya kiasi cha kwamba alishindwa kunyonyesha bintiye.

•Amesema kuwa wazazi wake pamoja na baadhi ya marafiki na mashabiki walimsaidia sana kupambana na msongo wa mawazo ambao ulikuwa umemuathiri.

Carrol Sonnie katika studio za Radio Jambo

Mwigizaji Caroline Muthoni almaarufu Carrol Sonnie alilemewa na hisia studioni zetu alipokuwa anasimulia kuhusu athari za baada ya kutengana na aliyekuwa mpenzi wake mchekeshaji Mulamwah.

Akizungumza na Massawe Jappani katika kitengo cha 'Ilikuaje?', Muthoni alikiri kuwa matukio yaliyofuata baada ya kutangaza kutengana kwake na Mulamwah yalimuathiri vibaya kiasi cha kwamba alishindwa kunyonyesha bintiye.

"Kusema kweli, sasa nimepona. Iliniathiri sana. Ilifika wakati hata singeweza kunyonyesha mtoto. Maziwa ilikuwa imeisha. Mamangu alikuwa anachukua simu yangu ili nisisome jumbe. Niliathiriwa na msongo wa mawazo. Ni mwanamke tu ataweza kuelewa hali hiyo. Nashukuru kuwa mtoto wangu anaendelea vizuri lakini hapo awali ilikuwa ngumu kwake," Muthoni alisema.

Muthoni alisema wazazi wake pamoja na baadhi ya marafiki na mashabiki walimsaidia sana kupambana na msongo wa mawazo ambao ulikuwa umemuathiri.

Mwigizaji huyo ameweka wazi kuwa tayari ameweza kusonga mbele na maisha yake. Hata hivyo amekiri kuwa anampeza sana Mulamwah katika maisha ya binti yao.

"Kusema kweli nilitaka mahusiano  yetu yafanye kazi. Lakini kwa kuwa mambo yalienda jinsi yalivyoenda lazima tusonge mbele na maisha na tuzoee. Napeza uwepo wake hasa kwa maisha ya mtoto wangu. Ningependa ahusike zaidi katika malezi," Muthoni alisema.

Mama huyo wa mtoto mmoja amefichua kuwa kwa sasa hawazungumzi na baby daddy wake. Pia alifichua kuwa mara ya mwisho ya Mulamwah kuona bintiye na akiwa na umri wa miezi miwili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved