logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Jamaa aachwa msimu wa Krismasi baada ya kumuambia mkewe "tumia akili"

Njoroge alisema kuwa aligombana na mama huyo wa mtoto wao mmoja na kimzaha tu akamwambia atumie akili.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri10 January 2023 - 05:40

Muhtasari


•Njoroge alisema kuwa aligombana na mama huyo wa mtoto wao mmoja na kimzaha tu akamwambia atumie akili.

•Maryanne alipopigiwa simu alimuambia Njoroge apige hatua ya kuenda nyumbani kwao ili waweze kusuluhisha.

Ghost na Gidi

James Njoroge ,35, alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mke wake Maryanne Njeri ambaye alitoroka mwezi Desemba

Njoroge alisema mkewe aligura ndoa yao ya miaka mitano takriban siku tatu kabla ya Krismasi kufuatia matatizo ya mawasiliano.

Alisema kuwa aligombana na mama huyo wa mtoto wao mmoja na kimzaha tu akamwambia atumie akili.

"Vile nilimuambia mke "atumie akili akifanya mambo yake" alichukulia kama ni matusi na akatoroka," alisema.

Alisema kuwa baadaye alipozungumza na Maryanne alimuarifu kuwa anapanga kwenda kufanya kazi Qatar.

"Aliniambia anataka kuenda Qatar aachie mamake mtoto. Mwishoni wa mwaka jana alikuwa ameniambia anataka kuenda kazi huko," alisema.

Njoroge alisema juhudi za kutatua mzozo wao hazijafanikiwa kwani mkewe amekuwa akikata simu zake.

"Dadake mkubwa alisema ata yeye hamuelewi  kabisa," alisema.

Maryanne alipopigiwa simu alimuambia Njoroge apige hatua ya kuenda nyumbani kwao ili waweze kusuluhisha.

"Si nilikwambia ukuje nyumbani," alimwambia kabla ya simu kukatika.

Njoroge alisema kwamba atafuatilia zaidi na kuenda kwa kina Maryanne.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved