logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Mimi ni mzuri kwa kupokea watu,'Hamisa azungumzia kurudisha uhusiano na Zari

Alipouliza kama kuna siku itakaja tokea wawili hao wawe marafiki alisema kuwa,

image
na Radio Jambo

Burudani16 October 2020 - 10:17

Muhtasari


  • Nina matumaini tupatane ili watoto wajuene kwa maana ni wa baba mmoja
  • Mimi ni mtu ambaye huwaga mzuri sana kwa kupokea watu
  • Tuna matumaini huko mbele kutakuwa sawa licha ya changamoto ambazo tunapitia
HAMISA-MOBETTO

Hamisa Mobetto ambaye ni baby mama wake staa wa bongo Diamond ameweka mambo wazi huku akisema yuko tayari kupatana na Zari Hassan na kurudisha uhusiano wao.

Akiwa kwenye mahojiano Hamisa alisema kuwa ni mzuri kwa kuwapokea watu na yuko tayari kuweka amani kati yake na Zari kama vile yuko na uhusiano na aliyekuwa mpenzi wake Diamond Tanasha Donna na Wema Sepetu.

Alipouliza kama kuna siku itakaja tokea wawili hao wawe marafiki alisema kuwa,

 

"Kama itakuja kutokea, mimi I’m here. Mimi ni mtu ambaye huwaga ni mzuri sana kwenye kupokea watu, na mkarimu. Kwa hiyo kama imepangwa, kama itakuja kutokea sawa I’ll be here.” Alizungumza Hamisa.

Hamisa alipoulizwa kama baby mama wa staa wa bongo Diamond wamepanga au watapanga wawakutanishe watoto wao ili wajueni mama huyo alisema anamatumaini kuwa yatatendeka.

zari

“When it comes to kids ambao wana baba mmoja kila mtu anahope familia zikutane vitu viwe vimoja, kila mtu awe ni kitu kimoja tuzidi kusogesha mbele kwa hiyo kama kuna any circumstances ama shida, we are hoping huko mbeleni kuwe sawa."

Mbali na kuwa rafikiye Wema na Tanasha bado ugomvi upo kati yake na Zari Hassan ambaye ana watoto wawili wa Diamond.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved