logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jiboresheni ! acheni kulalamika kila mara ,Churchill awashauri Zeddy na wachekeshaji wengine

Churchill amekua ajikipata pabaya kila wakatyi mchekeshaji anapojipata tabaan

image
na Radio Jambo

Habari29 October 2020 - 12:58

Muhtasari


  •  Churchill amekua ajikipata pabaya kila wakatyi mchekeshaji anapojipata tabaani
  •  Baadhi ya wasanii hujipata mashakani wakati pesa haziambatani na sifa ama umaarufu 
  •  Churchill alitumia mazishi ya Othuol kutoa ushauri wake 

   Mchekeshaji Churchill yaonekana amechoshwa na sarakasi za baadhi ya wasanii ambao aliwapa fursa katika jukwaa lake wajijenge lakini wakati wote wamekuwa wakitoa cheche za maneno na shutuma wakati wanapopatikana mashakani .

 Wakati wa mazishi ya mchekeshaji Othuol Othuol Churchill aliamua kusema yote moyoni kwa kumtaka Jalangó kutafsiri hotuba yake .

 Churchill aliwataka  wachekeshaji wenzake kujijenga  na kukoma tabia ya kenda katika mitandao ya kijamii kuwaambia mashabiki wao kila jambo linalofanyika katika maisha yao .

 

 ‘Acheni kuwaita mashabiki wenu familia …wakati utakaposhindwa kuwachekesha basi hutakuwa tena familia . Acha kuamka kila siku na kuwaambia kuhusu ulichokula ,ulivyovalia..acheni!’alisema Churchill

Zeddy  ambaye amekuwa chini ya Churchill katika fani ya ucheshi  amekuwa akigonga vichwa vya habari kwa  msimamo wake wa kueleza masaibu wanayopitia wachekeshaji wenzake . Amekuwa akisema kwamba wengi wao wana matatizo ya fikra kwa sababu ya shinikizo inayoambatana na  kazi yao ya kuangaziwa katika runinga na vyombo vya habari .

  Wakati Churchill alipokuwa akizungumza na wenzake katika fani ya burudani alimgeukia Zeddy na kumuambia

" Unaniskia Zeddy? Achana na wanablogi ,wanapata pesa kupitia stories zako .Jikuuze pamoja na brandi yako na pesa zitakufuata’

           

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved