Maceleb wanawake wakenya ambao hawajaolewa

Muhtasari
  • Wanawake maceleb wakenya ambao hawajaolewa 
Wilbroda
Wilbroda

Si wanawake wote ambao ni maceleb na wameweza kufunga pingu za maisha, ndio kuna wale walikuwa wamefunga pingu za maisha na kisha wakepeanaa talaka lakini hawajaweza kufanikiwa tena kuolewa.

Huwa tunawaona kenye mitandao ya kijamii, wakitufurahisha na hata wakiwashauri wanamitandao.

Hii hapa orodha ya wanawake wa kenya amabo ni maceleb lakini wamo single.

 

1,Jackline Nyaminde

Aliyekuwa muigizaji wa kipindi cha Papa Shirandula na ambaye ni mtangazaji, amebarikiwa na mtoto mmoja huku akiwa bado hajaingia kwenye ndoa.

Nyaminde alifahamika sana kama Wilbroda wakati wa uigizajii wake.

Awali akiwa kwenye mahojiano Nyaminde alisema kuwa alitoka katika uhusiano wake wa ndoa mara ya kwanza kwa maana ilikuwa ndoa yenye sumu na isiyo na amani

2.Betty Kyallo

Mwanabiashara huyo amuwa akitazamiwa sana na vijana wengi kwa bidii yake katika kazi na biashara yake, Betty waitengana na mumewe miezzi sita baada ya kufunga pingu za maisha.

Betty amebarikiwa na mtoto mmoja huku akiwa bado hajaingia katika ndoa tena.

 

3.Shix Kapienga

Ni celeb ambaye alifamika sana alipokuwa mtangazaji wa kampuni ya Royal media, huku akiwa bado hajapata mumewe wa maisha.

4.Melody Sinzore

Ni mtangazaji wa runinga a Citizen katika kipindi cha roga roga cha kila jumamosi, Melody anafahamika sana kwa densi zake za nyimbo za rhumba.

5.Terry Muikamba

Ni mtangazaji wa redio ya classic 105, mtangazaji huyo bado hajafanikiwa kupata mumewe.