logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Hii mapenzi ya mitandaoni utapata nyumbani ni vita,'Mashabiki wamwambia Bahati na Diana Marua

Kupitia kwenye mitandao ya kijamii ya instagram Bahati aliposti picha na kuandika ujumbe

image
na Radio Jambo

Habari23 November 2020 - 06:13

Muhtasari


  • Diana Marua na mumewe Bahati wapokea kejeli kutoka kwa mashabiki
dm

Kwa muda sasa msanii Kevin Bahati na mkewe Diana Marua wamekuwa wakipakia picha si haba kwenye mitandao ya kijamii huku baadhi ya mashabiki wakiwapongeza na wengine wakiwakejeli.

Kupitia kwenye mitandao ya kijamii ya instagram Bahati aliposti picha na kuandika ujumbe kuwa yeye na mkewe hawakosani ilhali kunamsemo unaosema wakosanao ndio wapendanao.

"Wanasema Wakosanao Ndio Wapendanao... Sisi Hatukosanangi Aki Nabado Tunapendana 😆 ARE WE OKEY???" Bahati Aliandika.

Wakati huo Diana aliposti picha hiyo kwenye ukurasa wake huku akipokea kejeli kutoka kwa mashabiki.

Baadhi yao walimwambia kuwa upendo ambao wanawaonyesha mashabiki kwenye mitandao ya kijamii utapata kuwa nyumbani hamna upendo huo.

Huku wengi walisem kwamba wawili hao wamezidi na kujigamba kwenye mitandao hiyo.

Hizi hapa baadhi ya hisia za wanamitandao;

Gracie Grace: Hii mapenzi ya social media utapata hta sio ya ukweli kwanyumba 😂😂.. ogopa soshomedia

Ruphy Michael: Nikiwa mkubwaa nataka kuwa kama nyinyi

Heis Nuby: na baha ni mdogo kweli anaonewaaa😢

 
 

Wanjiru Cate: Tunajua mnapendana si muache hii kushoiinda kupost... mmezidi sasa pia nyinyi


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved