logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Siamini maisha ya ndoa, kwa maana nilipitia dhuluma za kijinsia-Karen Nyamu

"Napenda watoto, na ninapenda watoto wangu lakini siamini ndoa

image
na Radio Jambo

Habari13 January 2021 - 10:37

Muhtasari


  • Karen Nyamu afichua kunawakati alidhulumiwa na aliyekuwa mumewe

Mwanasiasa Karen Nyamu akiwa kwenye mahojiano na radiojambo alisema kwamba hana imani yeyote katika ndoa hii ni baada ya kudhulumiwa kijinsia awali akiwa kwenye ndoa.

Nyamu ambaye alidaiwa kuwa na uhusiano na mwanamuziki Samidoh alisema kwamba alikuwa kwenye ndoa ambapo mumewe alimdhulumu na hakutaka azungumze naye.

"Napenda watoto, na ninapenda watoto wangu lakini siamini ndoa kwa maana nikiwa na mia ishirini nilidhulumiwa na aliyekuwa mume wangu

 

Sikuripoti kwa polisi kwa maana alikuwa mwanasiasa wakati huo, nilikuwa nafanya kazi kwa kampuni yake

Alihisi kuwa anaweza niambia kila kitu, lakini wakati huo hakujue hangeweza kunielekeza au 'kunicontrol'

Nina akili na mawazo kuwa naweza jisimamia kwa kila kitu, pia nilihisi nikienda kuripoti kwa kweli hamna kitu ingetendeka kwa maana alikuwa mtu ambaye alikuwa anajulikana sana." Aliongea Karen.

Karen ambaye aliwania kiti cha mwakilishi wa wanawake wa kaunti ya Nairobi mwaka wa 2017, alipoulizwa kwanini hakutoka katika ndoa hiyo mapema alisema kwamba mwanasias huyo alikuwa anamtishia maisha.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved