logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Naogopa mimba kuliko corona- msanii Akothee akiri

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagrama Akothee alikiri kwamba anaogopa mimba

image
na Radio Jambo

Yanayojiri26 January 2021 - 09:54

Muhtasari


  • Msanii Akothee akiri kitu ambacho anaogopa wakati huu wa sasa, kuliko corona

Kwa kweli nani hamfahamu msanii Esther Akoth almaarufu Akothee humu nchini, kwa ajili ya sifa zake tofauti.

Wengi wanamfahamu kama 'president of single mothers'. kwa ajili ya kukuza watoto wake pekeyake.

Msanii Akothee ana hadithi ya kusisimua kuhusu safari yake ya usanii, na hata ya kuwa mzazi.

 

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagrama Akothee alikiri kwamba anaogopa mimba kuliko virusi vya corona.

Huku akiendelea kusimulia Akothee alisema kwamba corona unaweza ambukiza watu wasipovaa maski.

Msanii huyo aliwashauri mashabiki wake waache abebe mimba kwenye ndoto kwa maana wanaume wa siku hizi wamekuwa wakiteleza kama sabuni.

"Niacheni Nibebe mimba kwenye Ndoto tafathali, kila mtu amekubaliwa kuota ,niacheni note πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ€¦πŸ€¦Mimba yaweza kufanya ukawa mlevi hata KWA kunywa maji tuu.πŸ˜‚πŸ’ƒπŸ’ƒπŸ’ƒπŸ’ƒπŸ’ƒπŸ’ƒ." Aliandika Akothee.

Kwa kweli wewe unaogopa nini maishani, tayari madam boss ameweka wazi nini haswa anaogopa wakati huu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logoΒ© Radio Jambo 2024. All rights reserved