logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Orodha ya wasanii bora mwaka wa 2021(Maoni)

Lakini je kulingana na maoni yako nani anapaswa kuwa msanii bora mwaka wa 2021 kati ya wasanii hawa.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri04 February 2021 - 11:44
Nadia-2-e1566897594626-696x395

Tasnia ya muziki kwa mara nyingine imeonekana kuinuka kwa mara tena baada ya wasanii tofauti kujitolea na kutoa vibao vipya kila kuchao.

Kuna baadhi ya wsanii ambao wamewafurahisha mashabiki wao kwa ajili ya bidii ambayo wanayo katika kazi yao.

Lakini je kulingana na maoni yako nani anapaswa kuwa msanii bora mwaka wa 2021 kati ya wasanii hawa.

 

1.Nadia Mukami

Ni msanii wa kike ambaye ameonyesha bidii kubwa kwenye tasnia ya usanii licha ya yake kuwa mwanamke.

Nadia amekua akitoa kibao kimoja baada ya kingine huku akiwashirikish wasanii wenzake.

2.Otile Brown

Amekuwa kwenye tasnia ya muziki kwa muda sasa huku akitoa kibao kimoja baada ya kingine.

Otile Brown

Mapema wiki jana Otile alitoa kibao cha siku ya wapendanao yaani 'Valentines'.

3,Mejja

 

Msanii Meja mtoto wa Khadija amekuwa akivuma kila mara endapo kibao kipya kimetolewa, amekuwa kwa tasnia ya muziki kwa zaidi ya miaka kumi sasa, hivi majuzi Mejja ametoa kibao ambacho kinafahamika kama 'Ulimi Wangu'.

Mejja na Massawe Japanni studioni

4.Willy Paul

Ni msanii ambaye amekuwa akisonge na mbele licha ya kupokea ukosoaji mkubwa na kejeli kutoka kwa mashabiki.

Tumemuona hivi majuzi akiwa amemsajili msanii katika lebo yake na kutoa kibao kipya.

Willy Paul

Swali kuu ni je ina maana wasanii wa kike wamelemewa na kazi hii ya usanii au wapo wapi?

Kulingana na maoni yako ni msanii yupi ambaye ameanza vyema mwaka huu na anapaswa kuwa msanii bora wa mwaka wa 2021.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved