logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maisha ya kila mtu yana misimu wakati wako ukifika ng'aa-Ushauri wake Grace Ekirapa

Grace alisema kwamba maisha ya kila mtu yana misimu wake.

image
na Radio Jambo

Burudani08 April 2021 - 12:11

Muhtasari


  • Grace na mumewe Pascal Tokodi hawajakuwa na aibu wakizungumzia ndoa yao, wala changamoto wamepitia awali kabla ya umaarufu wao
  • Grace alisema kwamba maisha ya kila mtu yana misimu wake

Mtangazaji Grace Ekirapa kupitia kwenye ukurasa wake wa mitandao ya kijamii ya instagram amekuwa akiwapa mashabiki wake nguvu na ushauri wa kuendelea na maisha.

Grace na mumewe Pascal Tokodi hawajakuwa na aibu wakizungumzia ndoa yao, wala changamoto wamepitia awali kabla ya umaarufu wao.

Kupitia kwenye ukurasa huo huo aliwashauri mashabiki wake kama wakati wa mtu wa kung'aa umefika anapaswa kung'a kulio awali.

 

Pia alisema kwamba kuna wale hutumia wakati kujaribu kupunguza mwanga wa watu wengine kwa sababu tu wanaogopa kung'arisha wao wenyewe.

Grace alisema kwamba maisha ya kila mtu yana misimu wake.

"Maisha ya kila mtu yana misimu. Wakati  wako ukifika, ng'aa kama hapo awali. Usifiche taa yako kwa sababu mtu fulani anatishwa nayo

Watu wengi hutumia wakati kujaribu kupunguza mwanga wa watu wengine kwa sababu tu wanaogopa kung'arisha wao wenyewe

Kumbuka, msimu huo utapita, kwa hivyo fanya sasa au milele ubaki kuwa kivuli nyuma ya nuru ya watu wengine

Zingatia pia kung'arisha na usijali ni nani taa  yake ni nyepesi kuliko yako au nani utazima taa yake kwa sababu hiyo ni kazi mingi ️ Kuwa na siku ya kung'aa 😊😊," Aliandika Ekirapa.

Swali kuu ni je umechukua msimu wako wa kung'aa au umeacha umekupita?

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved