logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilichukia macho yangu kwa maana ni makubwa-Muigizaji Nyce wanjeri

Muigizaji Nyce wa Njeri almaarufu Shiro, alifahamika kupitia kwa uigizaji wake katika kipindi cha 'Auntie Boss'.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 April 2021 - 09:46

Muhtasari


  • Katika kila mwili wa mwanadamu kuna sehemu au kiungo cha mwil ambacho huona Mungu hakufanya vyema na kukichukia
  • Nyce alisema kwamba alikuwa anachukia Macho yake kwa maana ni makubwa, kwani hakujua yatakuja kuwa faida kwake wakati wa uigizaji
Shiro-Auntie-Boss

Katika kila mwili wa mwanadamu kuna sehemu au kiungo cha mwil ambacho huona Mungu hakufanya vyema na kukichukia.

Baadhi ya wasanii, waigizaji kupitia kwenye kurasa zao za instagram wamekuwa wakizungumzia kiungo ambacho wanachukia au walikuwa wanakichukia walipokuwa wakikua.

Muigizaji Nyce wa Njeri almaarufu Shiro, alifahamika kupitia kwa uigizaji wake katika kipindi cha 'Auntie Boss'.

Nyce alisema kwamba alikuwa anachukia Macho yake kwa maana ni makubwa, kwani hakujua yatakuja kuwa faida kwake wakati wa uigizaji.

"Nilichukia macho yangu kwa maana ni makubwa, na nilikuwa aaah okey mimi bado ni mwembamba sasa ni mali yangu katika uigizaji," Aliandika Nyce.

Pia muigizaji ambaye anafahamika sana kama Monica, Brenda Wairimu aliweka wazi kwamba alichukia midomo yake lakin baadaye ilikuja kuwa faida kwake.

"Nilichukia midomo yangu ikikua,mwishowe ilikuwa sababu yangu ya kupata kazi hii, kuna unzo hapo na mahali," Aliandika Brenda Wairimu.

Somo kuu au jambo kuu la kujifunza ni kwamba hata kama unachukia nini katika mwili wako, kumbuka kuna sababu ambayo Mungu alikuumba jinsi ulivyo.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved