logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize achorwa tattoo ya uso wa hayati Magufuli kwenye mguu wake

Baadaye alipakia picha huku mashabiki wakitoa hisia tofauti.

image
na Radio Jambo

Habari30 April 2021 - 09:49

Muhtasari


  • Harmonize achorwa tattoo ya uso wa hayati Magufuli kwenye mguu wake
  • Msanii wa bongo Harmonize ni msanii ambaye amekuwa akikejeliwa sana mitandaoni kwa ajili ya vitendo vyake

Msanii wa bongo Harmonize ni msanii ambaye amekuwa akikejeliwa sana mitandaoni kwa ajili ya vitendo vyake.

Siku chache zilizopita alitoa kibao huku akimshirikisha Awilo Longomba huku akivunja rekodi ya staa wa bongo Diamond.

KUpitia kwenye mitandao ya instagram Harmonize alipakia video akichorwa mchoro wa tattoo wa uso wake hayati John Pombe Magufuli.

 

Baadaye alipakia picha huku mashabiki wakitoa hisia tofauti.

KUlingana na Harmonize aliamua kuchora uso wake mwendazake Magufuli ili kumuomboleza na kumkumbuka.

Kwenye tattoo yake aliandika maneno haya;

"Mimi nime sacrifice Maisha yangu Kwaajili ya Watu Maskini”. R.I.P KAMANDA," ujumbe ulisoma.

Kulingana na mashabiki wengi ni kuwa msanii huyo anapenda sifa na kiki nyingi katika maisha yake.

Maoni yako ni yapi kuhusu tattoo yake Harmonize je amefanya jambo nzuri au ni sifa tu anatafuta?

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved