- Siku ya JUmatatu ilikuwa ni furaha kwa watahiniwa wa mtihani wa kidoto cha nne K.C.S.E baada ya matokeo yao kutangazwa na waziri wa elimu George Magoha
Siku ya JUmatatu ilikuwa ni furaha kwa watahiniwa wa mtihani wa kidoto cha nne K.C.S.E baada ya matokeo yao kutangazwa na waziri wa elimu George Magoha.
Baadhi ya wanafunzi waliojizolea alama nzuri walisheherekea huku wanafunzi 893 wakijizolea alama ya 'A'.
Wanafunzi waliopata alama nzuri walisheherekea kwa njia tofauti huku baadhi ya watu mashuhuri wakiwasheherekea watoto wao waliofanya vyema.
Baadhi ya watu hao ni aliyekuwa muigizaji wa kipindi cha Papa Shirandula Njoro, aliyekuwa gavana wa nairobi Mike Sonko, seneta wa zamani Bonnie Khalwale na wengineo.
1.Njoro
Muigizaji huyo alisheherekea mwanawe kwenye ukurasa wake wa instagram huku akifichua kwamba mwanawe alijizolea alama ya B- huku akimshukuru Mungu.
"Asante kwa Mungu, maombi yako hayakuwa ya bure,tumepata alama ya B- najivunia sana sasa jiunge na mimi," Aliandika Njoro.
2.Mike Sonko
NI mwanasiasa ambaye amekuwa akiwasaidia wananchi, huku akijivunia kuwa mwanawe alijizolea alama ya B-
Pia alifichua kwamba katika mtihani wake wa darasa la nane alipata alama 399, huku akijiunga na shule ya upili ya Lenana.
3.Bonnie Khalwale
Mwanasiasa huyo alitangaza matokeo ya mwanawe kupitia kwenye ukurasa wake wa twitter aliyejizolea alama ya B+
Hongera kwa watahiniwa ambao walipita mtihani wao wa kidato cha nne, kweli hawakukosea mchumia juani hulia kivulini