Msanii na Rappa wa humu nchini Kaligraph Jones siku ya JUmamosi Mei 15, alipeleka msaada wa chakula katika eneo la Kayole kaunti ya Nairobi.
Haya yanajiri wiki chache baada ya msanii huyo kukutana na naibu rais William Ruto na kumpa vilio vya wasanii na vile wanateseka.
Wakati huu wa janga la corona wengi wa wananchi wamepoteza makazi yao na hata wengi kupitta wakati mgumu.
Kupitia kwenye uurasa wake wa instagram msanii huyo alipakia picha huku akiwa amesimama na watoto tayari kusambaza chakula.
Pia kwenye mitanda hiyo hiyo alipakia video huku watu wakipokea unga.
Huu hapa ujumbe wake rappa huyo;
"Leo Ilikuwa Siku Njema, tuliweza Kutoa Kitu Kidogo Kwa watu wasiojiweza wakati wa nyakati hizi ngumu za Corona. Asantenyote kwa kuheshimu OG .." Aliandika JOnes
Msanii huyo alilelewa mtaa wa Kayole hivyo basi aliwasaidia watu wa mtaa wake kuwahakikishia kwamba hajawasahau hasa wwakati huu mgumu.