logo

NOW ON AIR

Listen in Live

''Si mwanaume wa kawaida, ni mfalme" Milly amsifu Kabi

Wanandoa Kabi na Milly Wajesus waendelea kushangaza wengi na mapenzi kati yao licha ya changamoto zilizokumba ndoa yao hivi majuzi

image
na Radio Jambo

Burudani25 May 2021 - 06:35

Muhtasari


“Nakupenda sana malaika. Bila wewe mimi ni mvulana mdogo tu na paji la uso kubwa na nywele kwa mguu, unanikamilisha” Kabi alimuandikia Milly.

Kabi na Milly Wajesus

Wanandoa Peter Kabi (Kabi Wajesus)  na Millicent Wambui(Milly Wajesus) wameendelea kuwashangaza wengi kutokana na mapenzi wanayoonyesha mitandaoni licha ya masaibu yaliyokumba ndoa yao wiki chache zilizopita.

Siku ya Jumatatu, Milly alimsherehekea mumuwe kwa ujumbe wa kusisimua huku akimsifia kuwa anayependa sana, mcha Mungu na mwenye bidii sana.

“Si mwanaume wa kawaida, yeye ni mfalme. Ni mtu anapenda kuomba, anajua kupenda na mwenye bidii sana. Najivunia sana kumuita mume wangu." Milly aliandika huku akimuarifu mumewe.

Kwa upande wake Kabi, alimuambia Milly kuwa anampenda sana na anamkamilisha kama mwanaume.

“Nakupenda sana malaika. Bila wewe mimi ni mvulana mdogo tu na paji la uso kubwa na nywele kwa mguu, unanikamilisha” Kabi alimjibu Milly.

ujumbe wa Kabi

Wengi mitandaoni walimsuta sana Kabi kwa kukiri kuwa ana mtoto na binamu yake huku wengine wakikadiria kuwa huo ni mwisho wa ndoa ya wawili hao. Hata hivyo, wapenzi hao wameendelea kuthibitishia makosa wanaowatilia shaka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved