logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nyota Ndogo akashifu wanaosema ni pesa tu anataka

"Mna ushenzi sana roho zenu za korosho kuchomwa!" Nyota ndogo awasuta wanaokejeli hali yake

image
na Radio Jambo

Habari26 May 2021 - 03:48

Muhtasari


• Nyota Ndogo amekasirishwa sana na madai kuwa ni pesa za mpenzi wake mzungu tu anataka ila si mapenzi.

•Alikiri kuachwa na mpenziwe mwezini Aprili amekuwa akichapisha jumbe za kumwagiza mumewe kumrudia kwenye mtandao wa Instagram huku akidai kuwa amefungiwa namna yote anayoweza kumfikia nayo.

Nyota Ndogo na mumewe

Mwanamuziki Nyota Ndogo ameonekana kukasirishwa sana na madai kuwa ni pesa za mpenzi wake mzungu tu anataka ila si mapenzi.

Msanii huyo toka Pwani amewasuta wale ambao wamekuwa wakikejeli hali yake huku akiwaarifu kuwa hana haja na pesa za wenyewe kwani anajua kujitafutia.

"Hee Wakenya jamani mimi nimeshachoka kusema najua kusaka pesa zangu kwa njia iliyo sawa ila uvivu wenu umefanya mnaona kila mtu mvivu. Lakini nani hapendi hela? Mna ushenzi sana roho zenu za korosho kuchomwa. Mnatamani kila mtu awaombe ili mumseme. Haya,nataka hizo za Mungui mimi simushukuru siwaombi jamani!" Nyota Ndogo aliandika huku akizungumziwa ripoti iliyodai kuwa analilia pesa tu.

Nyota Ndogo ambaye alikiri kuachwa na mpenziwe mwezini Aprili amekuwa akichapisha jumbe za kumwagiza mumewe kumrudia kwenye mtandao wa Instagram huku akidai kuwa amefungiwa namna yote anayoweza kumfikia nayo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved