logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Achana na mabibi zangu,'Eric Omondi amwambia Ringtone, msanii huyo amjibu

Omondi aliweka wazi wakati huu lazima ampate bibi, na mpenzi wake wa maisha.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri02 June 2021 - 14:12

Muhtasari


  • Mchekeshaji Eric amsihi Ringtone asifanye haya

Je kipindi cha mchekeshaji Eric Omondi kitarejea? ni swali ambalo wanamitandao wamesalia nalo vichwani mwao baada ya Eric Omondi kusema kwamba anatarajia kuwaleta wanawake warembo nchini.

Hii ni baada ya kumuonya msanii wa nyimbo za injili awachane na wanawake wake, kwani hivi karibuni anawaleta wanawake kutoka Sudan kusini,Rwanda,Nigeria na Ethiopia.

Omondi aliweka wazi wakati huu lazima ampate bibi, na mpenzi wake wa maisha.

"Rais lazima aunge mkono muziki mzuri. Huyu Kijana ako na na wito wa juu na kipawa kutoka juu mbinguni...Shida tu ni awachane na mabibi zangu...niko karibu kuwaleta wanawake warembo nchini kenya kutoka  ETHIOPIA, RWANDA, SUDAN KUSINI na NIGERIA bwana CHAIRMAN tafadhali usiwafagie kwa sababu wakati huu lazima nipate mke. Naomba," Aliandika Eric.

Kw aupande wake msanii Ringtone, alimjibu na kumwambia kwamba hana haja na wanawake wake.

"Ndugu yangu, sina biashara yeyote, ya kuwaiba wake wako," Alimjibu Ringtone.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved