logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+VIDEO)Ombeeni mtoto wangu apone-Baba yake DJ Evolve azungumza

Kwenye video iliyotolewa kwa vyombo vya habari, baba ya DJ Evolve alisema alikuwa na huzuni

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 June 2021 - 11:31

Muhtasari


  • Kwenye video iliyotolewa kwa vyombo vya habari, baba ya DJ Evolve alisema alikuwa na huzuni kusikia kwamba watu wangetamani kifo juu ya mtoto wake
DJ 1

Baba wa mcheza santuri  DJ Evolve John Orinda ameelezea kusikitishwa kwake na ripoti kwamba mtoto wake ameaga dunia

Kwenye video iliyotolewa kwa vyombo vya habari, baba ya DJ Evolve alisema alikuwa na huzuni kusikia kwamba watu wangetamani kifo juu ya mtoto wake.

"Chochote ninachosikia sio sawa, sio kweli. Nilishtuka kusikia ripoti kama hizo. Tunapoamka kila asubuhi, jambo la kwanza ni kumuona  mtoto wetu, kwa sasa anaendelea vizuri

Kila mtu anapaswa kumwombea tu, kwa sababu mmesema mnampenda, mwombee apone. Hivi sasa, maombi yenu yanafanya kazi Anaweza kukaa peke yake kwa muda wa saa moja, kisha hulala tena. Anaweza hata kukaa kwenye kiti kwa masaa 8. Tumuombee tu, alikuwa katika hali mbaya, lakini sasa anaendelea vizuri, "alisema John Orinda.

Ripoti juu ya kifo cha Evolve ziliibukana kuenezwa kupitia kwenye mitandao ya kijamii Jumanne saa sita.

Mara tu baada ya uvumi huo kuenea, sehemu ya Wakenya kumlaumu mbunge wa Embakasi mashariki Babu Owino.

Evolve alipatana na ajali yake mapema mwaka wa 2020, huku akilazwa hospitali kwa zaidi ya miezi 5 akipokea matibabu.

Hii hapa video akizungumza;


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved