logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Wanaume wa kenya ni 'Stingy'-Huddah Monroe

Mfanyabiashara huyo amekuwa akiishi nchini Dubai kwa muda huku akiendeleza biashara yake.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri15 June 2021 - 10:13

Muhtasari


  • Huddah Monroe afichua sababu hajawahi wachumbia wanaume wa kenya
Screenshot.from.2019.10.17.12.37.26

Mwanasosholaiti na mfanyibiashara Huddah Monroe kupitia mtandao wa kijamii wa instagram, kitengo cha maswali na majibu amewafungulia mashabiki wake roho yake.

Huddah amedai kuwa wanaume ambao amewahi chumbia maishani mwake kutoka Kenya hawapendi kutumia pesa kwa wapenzi wao.

Yaani wanaume 'stingy'.

Mfanyabiashara huyo amekuwa akiishi nchini Dubai kwa muda huku akiendeleza biashara yake.

"Nimewachumbia karibu wanaume wote wa aina yote duniani.  Chinese, India lakini kwa hakika najua wanaume kutoka Asia sio wa ligi yangu

Katika Afrika mwanamume kutoka Nigeria ni kuwa na maumivu ya kichwa, sio wabaya kwa kujivinjari lakini sio wa kuwa kwa ndoa nao labda ukitaka kufa ukiwa na umri mdogo

Maisha ni kuhusu uamuzi, hao pia sio wa ligi yangu,wanaume wa Kenya wanaweza kuwa 'stingy' sana mimi napenda kutumia pesa

Mwanamume ambaye anaongea french huyo ni wangu na wa ligi yangu," Huddah Aliandika.

 

(Mhariri: Davis Ojiambo) 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved