(Video) Kiki tu! Brown Mauzo apuuzilia mbali madai ya kutengana na Vera Sidika kwa wimbo

Siku ya Alhamisi Mauzo alitangaza kupitia mtandao wa Instagram kuwa angehutubia Wakenya kuhusiana na tukio lake kukosa kwenye sherehe hiyo mnamo Ijumaa(leo)

Muhtasari

•Mdahalo ulikuwa umeibuka mitandaoni kuwa wawili hao huenda walikuwa wamekosana licha ya wao kutesa wanamitandao kweli kwa picha na jumbe kochokocho za mapenzi kwa kipindi kirefu.

•Kweli mwanamuziki huyo kahutubia Wakenya ila ni kwa wimbo ambao unazungumzia safari ya ujauzito wa mkewe.

Image: INSTAGRAM

Masalale! Kumbe hatua ya mwanamuziki Brown Mauzo kukosa kuonekana kwenye sherehe ya kufichua jinsia ya mtoto aliyebeba mpenziwe Vera Sidika ilikuwa kiki tu!

Hii imebainika wazi baada ya mwanamuziki huyo toka Pwani kupakia kibao alichomtungia Vera kwenye mtandao wa YouTube siku kadhaa baada ya sherehe hio kufanyika.

Mdahalo ulikuwa umeibuka mitandaoni kuwa wawili hao huenda walikuwa wamekosana licha ya wao kutesa wanamitandao kweli kwa picha na jumbe kochokocho za mapenzi kwa kipindi kirefu.

Siku ya Alhamisi Mauzo alitangaza kupitia mtandao wa Instagram kuwa angehutubia Wakenya kuhusiana na tukio lake kukosa kwenye sherehe hiyo mnamo Ijumaa(leo0

Kweli mwanamuziki huyo kahutubia Wakenya ila ni kwa wimbo ambao unazungumzia safari ya ujauzito wa mkewe.

Tazama hapa;

Utanizalia is Brown Mauzo and his wife Vera Sidika latest single that talks about their pregnancy journey and the love they have for each other. UTANIZALIA ( Lyrics) verse 1 mahaba kina kirefu nlizama safari imefika mwisho nlikwama uuuh! wee ndo roho yangu uuuh! wee ndo mboni yangu nawapa wenye misemo mtaachana na dua njema atulinde Maulana uuuh wee ndo roho yangu uuuh wee ndo mboni yangu chorus x2 uliahidi utanizaliaa leo umebeba mimbaa kesho unanizalia ,inshallah ntampa nzuri jinaa mwanangu verse 2 Ah! nigandegande kama rubaa tuzeeke wawili leo na kesho wangu wa ubavuni tuzikwe wawili ushanchanganya,ewee mwaya, niko hoi mahututi wee ndo fire nlipagawa,nkachachawa Heyy! tulia apa tufe wote chorus x2 uliahidi utanizaliaa leo umebeba mimbaa kesho unanizalia ,inshallah ntampa nzuri jinaa mwanangu

Awali kabla ya kupakiwa kwa wimbo huo, Vera alikuwa ameandika ujumbe akiwasihi wanaume  kutofikiria 'kuhutubia wananchi' baada ya mambo kuenda mrama kwani  hakuna aliyefurahia utamu wa tendo la ndoa pamoja nao" Vera aliandika..

"Wanaume, ulipokuwa unamvua nguo, mlikuwa peke yenu. Hakuna ambaye alikuwa nanyi wakati mlikuwa mnafurahia utamu wa tendo la ndoa. Kwa hivyo usifikirie kuhutubia wananchi baada ya mambo kuenda mrama

Katikati mwa mwezi uliopita, mwanasoshalaiti huyo alitangaza wazi kuwa alikuwa akitarajia mtoto na mpenzi wake Brown Mauzo.

Matokeo ya vipimo yaliyotangazwa usiku wa Jumamosi yalithibitisha kuwa msanii huyo amebeba mtoto wa kike.