logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Hakuna atakayekuajiri kutokana na huruma!" Akothee awashauri 'single mums' wanaotafuta kazi

Madam Boss amewasihi 'single mums' kutoeleza masaibu yao wanapokuwa kwenye mahojiano ya kutafuta kazi.

image
na Radio Jambo

Habari19 July 2021 - 08:02

Muhtasari


•Mwanamuziki na mfanyabiashara mashuhuri nchini Akothee aliyebandikwa jina  Madam Boss amewasihi kina mama wasimbe (single mums) kutoeleza masaibu yao wanapokuwa kwenye mahojiano ya kutafuta kazi.

•Mama huyo wa watoto watano amewashauri 'single mums' wenzake wasiwahi geuza mahojiano ya kazi kuwa mahakama ya watoto.

Mwanamuziki na mfanyabiashara mashuhuri nchini Akothee aliyebandikwa jina  Madam Boss amewasihi kina mama wasimbe (single mums) kutoeleza masaibu yao wanapokuwa kwenye mahojiano ya kutafuta kazi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Akothee ambaye huwa anajitambulisha kama 'President of single mothers' amesema kuwa  waajiri huwa hawapatiani kazi kutokana na huruma ama mafadhaiko yaliyokumba mtu.

Mama huyo wa watano na ambaye anaaminika kuwa bilionea amewashauri 'single mums' wenzake wasiwahi kugeuza mahojiano ya kazi kuwa mahakama ya watoto.

"Ukiulizwa suala la mshahara wako, usianze kwa kusema eti 'unajua mimi ni single mother, nahitaji kulipa bili (haya ni mahojiano sio mahakama ya watoto). Hakuna atakayekuajiri kwa sababu ya huruma ama bili zako" Akothee alisema.

Mwanamuziki huyo amesema kuwa kampuni zinalipia thamani ya mtu ila sio wakati wake tu ama hali yake ya  kuwa mama.

"Zuia kutaja masaibu yako kwenye mahojiano na kuharibia mwajiri wako wa awali jina. Ukiulizwa mbona uliacha kazi yako ya awali sema kuwa unataka jukumu mpya na unahisi kwamba mandhari yale mapya yatakupatia nafasi ya kustawi na kuboresha utaalamu wako" Akothee alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved