logo

NOW ON AIR

Listen in Live

King Alami amuomba mpenzi wake Notiflow msamaha hadharani

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram wa King Alami alimuomba Notiflow msamaha

image
na Radio Jambo

Habari28 July 2021 - 11:50

Muhtasari


  • King Alami amuomba mpenzi wake Notiflow msamaha hadharani

Wiki chache zilizopita uhusiano wa kimapenzi wa  msanii Notiflow na mpenzi wake King Alami ulikwisha baada ya wawili hao kutengana.

Kulingana na Notiflow sababu yao ya kuacha ni kwa maana walichapana, huku akidai kwamba karibu aliyekuwa mpenzi wake amuue.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram wa King Alami alimuomba Notiflow msamaha kwa yote ambayo alimtendea.

Alami alikubali makosa yake na kusema kwamba alikuwa mkali kwa mpenzi wake.

"Nataka kuomba msamaha hadharani kwa mpenzi wangu @Notiflow, jambo la kwanza kwa kuwa mkali kwake, kumuumiza kimwili na kihemko

Jambo la pili kwa kumnyanyasa na kumpigia kelele, la tatu nilikuwa nataka kuweka haya hapa ili kutupilia mbali jinsi watu walichukulia mambo," Aliandika Alami.

Pia Notiflow aliweka wazi kwamba hawezi mrudia Alami kwa sababu ya tofauti zao na karibu amtoe uhai.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved