logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hutuwezi endelea kupoteza maisha kwa ajili ya kafyu,'Mchekeshaji MCA Tricky alaani unyama wa polisi

Tukio hilo lilitokea maeneo ya Tushauriane wakati marehemu alikuwa anaelekea nyumbani kwake.

image
na Radio Jambo

Burudani19 August 2021 - 14:27

Muhtasari


  • Mchekeshaji MCA Tricky alaani unyama wa polisi
  • Polisi wanadaiwa kumpiga jamaa mmoja hadi kifo kwa kukiuka amri ya kutotoka nje iliyowekwa kudhibiti maambukizi ya Corona

Maandamano yameshuhudiwa  siku ya Alhamisi katika mtaa wa Kayole wakazi wakilalamikia mauaji ya kiholelaholela yanayodaiwa kutekelezwa na maafisa wa polisi dhidi ya mmoja wao usiku wa Jumatano.

Polisi wanadaiwa kumpiga jamaa mmoja hadi kifo kwa kukiuka amri ya kutotoka nje iliyowekwa kudhibiti maambukizi ya Corona.

Tukio hilo lilitokea maeneo ya Tushauriane wakati marehemu alikuwa anaelekea nyumbani kwake.

Inaripotiwa kuwa mhasiriwa alikuwa amearifu mkewe kuhusu mateso aliyokuwa anapitia mikononi mwa askari waliokuwa wamemkamata  na hata kumtumia nambari ya gari lililokuwa limembeba.

Haya yanajiri wiki chache baada ya polisi Embu, kudaiwa kuwauwa ndugu wawili Emmanuel na Benson kwa kukiuka amri ya kutotoka nje.

Polisi hao walichukuliwa hatua na kuzuiwa kwa muda wa siku 14 ili uchunguzi ukamilike, sio mmoja au wawili bali baadhi ya wakenya wamewapoteza wapendwa wao baada ya kupitia mikononi mwa polisi.

Wakenya,wanamitandao,watu mashuhuri miongoni mwa wenine wanataka unyama wa polisi ukamilike.

Mchekeshaji wa churchill MCA Tricky kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amedai kwamba watu na wakenya hawatazzidi kupoteza maisha yao kwa ajili ya kafyu.

Pia ametaka ukatili, unyama wa polisi ukamilike haraka iwezekanavyo.

"#Kayole Polisi wanapaswa kuheshimu haki ya maisha, hatuwezi endelea kupotea maisha kwa ajili ya visingizio za amri ya kutotoka nje," Aliandika Tricky.

Wanamitandao walimuunga mkono na hizi hapa baadhi ya jumbe zao;

blacshady: So true vijana wanaisha😢😢

gounah23: Brutality must stop

samerigideon: La sivyo hata sisi tutaanza kuwa brutal kwao.

karenjonyunsuu: Together tukomeshe 😢

ronnyreagan5: SAY NO TO POLICE BRUTALITY. ENOUGH IS ENOUGH. ARISE YOUTHS AND FIGHT FOR WHAT YOU BELIEVE IN.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved