logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Juliani apiga ripoti baada ya kutishiwa maisha yake kwa kuchumbia aliyekuwa mke wa gavana Mutua

Mwanamuziki huyo alionywa dhidi ya kupakia picha alizopiga pamoja na Lilian kwenye mitandao ya kijamii na kutishiwa kuuawa iwapo angeendelea

image
na Radio Jambo

Habari02 September 2021 - 08:42

Muhtasari


•Mwanamuziki huyo alionywa dhidi ya kupakia picha alizopiga pamoja na Lilian kwenye mitandao ya kijamii na kutishiwa kuuawa iwapo angeendelea

Mwanamuziki Julius Owino almaarufu kama Juliani amepiga ripoti kuhusu vitisho dhidi ya maisha yake alivyopokea baada ya kuvunja kimya kuhusu uhusiano wake na Bi. Lilian Ng'ang'a.

Siku ya Jumatano mida ya jioni mwanamuziki huyo alifichua kuwa alikuwa amepigiwa simu na kutumiwa jumbe za vitisho punde baada ya kuzungumzia uhusiano wake na aliyekuwa mke wa gavana wa Machakos Alfred Mutua.

Mwanamuziki huyo alisema kuwa simulizi ya kunyang'anyana mke ni jambo la uongo na kusema kuwa hakuna vile mtu mzima anaweza 'kuibiwa'

"Unawezaje 'kuiba' mtu? Mtu mzima mwenye akili timamu! "Simu niliyopigiwa na ujumbe wa vitisho dhidi ya maisha yangu ambao nilipata leo sio jambo la kufurahisha! Simulizi ya 'Ulinyang'anyana ni ya uongo, ya kuchokesha na vichwa  tamu vya habari tu. Tafadhali wacheni" Juliani aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Kwenye ujumbe wake msanii huyo alimuagiza aliyekuwa anampa vitisho iwapo ataamua kuvitekeleza asiharibu sura yake kwani angependa kuzikwa akiwa anatabasamu.

"Kwa vitisho, usipime uso, ningependa kutabasamu ndani ya kaburi langu" Juliani alisema.

Mwanamuziki huyo alionywa dhidi ya kupakia picha alizopiga pamoja na Lilian kwenye mitandao ya kijamii na kutishiwa kuuawa iwapo angeendelea.

Adhuhuri ya Alhamisi Juliani  aliamka na kufululiza moja kwa moja hadi kituo cha polisi cha Kileleshwa ambapo alipiga ripoti na kuandikisha taarifa kuhusu vitisho hivyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved