logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Ninalinda nafasi yangu,'Muigizaji Sarah Hassan asema anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa

Pia Sarah amesema kwamba huwa analinda nafasi yake kwani ndio inamuweka.

image
na Radio Jambo

Burudani05 September 2021 - 08:50

Muhtasari


  • Muigizaji Sarah Hassan ni miongoni mwa waigizaji ambao wameigiza katika vipindi kadhaa nchini
  • Sarah aliahamika sana kupitia kwenye kipindi cha Tahidi High kilichokuwa kinapeperushwa kwenye runinga ya Citizen

Muigizaji Sarah Hassan ni miongoni mwa waigizaji ambao wameigiza katika vipindi kadhaa nchini.

Sarah aliahamika sana kupitia kwenye kipindi cha Tahidi High kilichokuwa kinapeperushwa kwenye runinga ya Citizen.

Sio kipindi hicho pekeyake balia anaigiza katika kipindi cha Zora kama Zora na muigizaji mkuu katika kipindi hicho.

Mama huyo wa mtoto mmoja huku akisherehekea siku yake ya kuzaliwa alipakia picha kwenye ukurasa wake wa instagram na kumshukuru Mungu kwa kumpa nguvu ya kufanya bidii katika kazi yake.

Pia Sarah amesema kwamba huwa analinda nafasi yake kwani ndio inamuweka.

"Yup, hiyo ni idadi kubwa ya wakati! Ninapenda vibes na nishati nzuri, kucheka, kucheza, tu kuwa na furaha!

Ninalinda nafasi yangu, ambayo inaniweka mimi, katika ulimwengu ambao unaweza kumfanya mtu ahisi kama hawafanyi kazi

Natumaini unalinda nafasi yako, kuweka nishati yako ya akili kwenye ngazi na natumaini unajua unatosha na unafanya kutosha!

Upendo na mwanga wa watu wazuri na furaha ya kuzaliwa kwa wenzangu," Aliandika Sarah.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved