logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Mungu nifariji, nipe nguvu" Mwanamuziki Size 8 amkumbuka marehemu mamake kwa ujumbe wa kihisia

Bi Esther Njeri Munyali aliangamia kutokana na matatizo ya figo mnamo mwezi Novemba mwaka wa 2015, masaa machache tu baada ya Size 8 kujifungua mtoto wake wa kwanza , Ladasha Belle.

image
na Radio Jambo

Habari15 September 2021 - 07:47

Muhtasari


•Bi Esther Njeri Munyali aliangamia kutokana na matatizo ya figo mnamo mwezi Novemba mwaka wa 2015, masaa machache tu baada ya Size 8 kujifungua mtoto wake wa kwanza , Ladasha Belle.

Mwanamuziki mashuhuri Linet Masiro Munyali alimaarufu kama Size 8 amemkumbuka marehemu mamake ambaye aliaga takriban miaka sita iliyopita.

Bi Esther Njeri Munyali aliangamia kutokana na matatizo ya figo mnamo mwezi Novemba mwaka wa 2015, masaa machache tu baada ya Size 8 kujifungua mtoto wake wa kwanza , Ladasha Belle.

Miaka sita baadae mwanamuziki huyo bado hajaweza kukabiliana na majonzi ya kupoteza mamaye mpendwa na kupitia ukurasa wake wa Instagram amemwomba Mola kumpa nguvu na faraja anapoendelea kuomboleza.

"Wakati ambapo mwanamke aliyekomaa anampeza sana mama yake waaah.. Mungu wa faraja yote naomba nifariji, nipe nguvu na neema yako inilinde na nguvu za kuendelea na safari hii kwani kwa nguvu zako naweza kuponda jeshi, nikiwa nawe naweza kupanda ukuta wowote" Size 8 aliandika.

Size 8 hakupata nafasi ya kumzika mama yake wakati aliaga kwani bado alikuwa amelazwa hospitalini akiwa anaugua sana.

Mamake Size 8  alizikwa katika mji wa Mbale nchini Uganda alikozaliwa bwanake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved