Rick Ross aweka wazi uhusiano wake na Hamisa Mobetto

Muhtasari
  • Rick Ross aweka wazi uhusiano wake na Hamisa Mobetto
Screenshot.from.2019.10.17.16.25.49
Screenshot.from.2019.10.17.16.25.49

Mwimbaji wa hip hop wa Marekani Rick Ross hatimaye  ameibuka na kuzungumzia uhusiano wake na Hamisa Mobetto.

Alithibitisha kuwa walikuwamarafiki wa karibu sana, wala hakufafanua ukaribu wa uhusiano wao huku akisema kwamba atamwachia Hamisa afafanue uhusiano wao.

Uvumi wa urafiki wao ulienea sana baada ya rappa huyo, kutoa maoni kenye picha za Hamisa alizokuwa anapakia kwenye ukurasa wake wa instagram, huku mashabiki wakisema kwamba wawili hao ni wapenzi.

Wawili hao pia walionekana karibu mwezi au miwili iliyopita huko Dubai na wanamitandao kudai wanaweza kuwa kwenye likizo.

Katika mahojiano na Lil Ommy, Rapa na mfanyabiashara aliyeshinda Tuzo aliongeza kuwa yuko tayari kumuunga mkono  Mobetto kutimiza ndoto zake zote kwa sababu yeye ni mjasiriamali mzuri.

"Lazima niseme ukweli, kuna uhusiano, ni kiasi gani unataka nitakuambia juu yake?, Nitamwachia yeye… lakini yeye ni mtu mzuri sana, mrembo roho na yeye ni mjasiriamali mkubwa na ninataka kumsaidia kuipeleka katika kiwango kingine kwa sababu anafanya kazi nzuri na ninajivunia.

Kuna mambo mengine kadhaa lakini yote kwa yote nataka kumuona akishinda ”alisema Rick Ross.

Rapa mkubwa wa Marekani, Rick Ross amefanya interview LIVE kwa njia ya Mtandao na Mtangazaji maarufu Tanzania, Lil Ommy, The King of Interviews na kuongea mengi kuhusu mpango wake wa kufungua tawi la lebo yake MMG (Maybach Music Group) Afrika, kuwa tayari kutumia lugha ya kiswahili kwenye nyimbo zake, kuwekeza Afrika, Tanzania, kutembelea Serengeti na mlima Kilimanjaro kwa muda wa wiki moja, Biashara zake na Belaire, Villon, Wingstop n.k Katika interview hii, Rozay The Boss amelezea mambo zaidi ya 10 yatakayokufanya ufanikiwe katika Maisha, pia ameongelea alivyofanya wimbo na Diamond Platnumz (waka waka, ilikuaje), ukaribu wake na Hamisa Mobetto, Drake, Belaire, Villon pamoja na Biashara zake Wings, Kumiliki magari zaidi ya 100, kununua magari ya zamani, Nyumba yake kutumika kwenye Movie ya Coming 2 America 2 (The Royal Palace). Rick Ross ameachana pia Grammy, amezungumzia kitabu chake kipya 'The Perfect day to Boss Up' jinsi anavyoamka asubuhi, vitu anavyofanya na kila kitu kuhusu Muziki na Maisha yake! Lil Ommy, amemuliza pia kuhusu kumiliki leseni ya gari akiwa ana magari zaidi ya 100 na hakuwa kuwa na leseni! Subscribe Channel hii, LilOmmyTV kuangalia full interview ambayo imewekea tafasiri ya kiswahili kwa uelewa zaidi. Like & Comment! Let's Connect http://www.instagram.com/lilommy http://www.twitter.com/LilOmmy https://mobile.facebook.com/lilommyfanpage https://wlo.link/@lilommy https://lilommy.com/ Subscribe, Stream, Share kwenye WhatsApp Groups au Facebook na Twitter.

Rick Ross pia alisema kuwa ana mpango wa kutembelea Tanzania hivi karibuni.