logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ukiwa kwa giza usiamini kila mwangaza unao uona-King Kaka kwa mashabiki

Hata hivyo alieleza kuwa ana matumaini ya kupata nafuu hivi karibuni.

image
na Radio Jambo

Habari15 September 2021 - 10:06

Muhtasari


  • Wiki chache zilizopita mwanamuziki  King Kaka alifunguka kwa umma juu ya ugonjwa wa ajabu amekuwa akipigana kwa miezi, ukimfanya apoteze kilo 33 kwa miezi mitatu

Wiki chache zilizopita mwanamuziki  King Kaka alifunguka kwa umma juu ya ugonjwa wa ajabu amekuwa akipigana kwa miezi, ukimfanya apoteze kilo 33 kwa miezi mitatu.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, King Kaka alifichua kuwa hajakuwa na hisia ya ladha kwa kipindi cha miezi miwili na amekuwa akila matunda na kunywa uji tu.

Kupitia kwenye ukurasa wake a instagram Kaka alimewashuri mashabiki wake kuto amini kila mwangaza wanao uona wakiwa kwenye giza.

"Ukiwa kwenye giza usiamini kila mwangaza unao uona," King Kaka aliandika.

Kaka alisema kuwa hata nguo alizokuwa anavaa hapo awali hazimtoshei kwa sasa kufuatia kupungua kwa ukubwa wa kiuno chake.

" Mashabiki wangu, nimeona ni heri niwaambie haya. Nimekuwa mgonjwa kwa miezi mitatu na siku nane. Nilipimwa vibaya. Nimepoteza kilo 33 kwa wakati huo na tulianza kutembea hospitalini. Nimefanyiwa vipimo vyote na hakuna matokeo. Cha kushangaza ni kuwa sina maumivu yoyote na tunatumai kuwa tutapata suluhu hivi karibuni. Kiuno changu kilikuwa na ukubwa wa 36 na sasa ni 33" King Kaka aliandika.

Hata hivyo alieleza kuwa ana matumaini ya kupata nafuu hivi karibuni.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved