logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Flaqo anatuharibia ndoa,'Kabi Wajesus amtania baada ya mkewe kumezea mchekeshaji huyo

Milly pia ni miongoni mwa wanawake ambao walipendezwa na misuli yake Flaqo

image
na Radio Jambo

Yanayojiri18 September 2021 - 06:19

Muhtasari


  • Kabi Wajesus adai Flaqo anaharibu familia yake
  • Kulingana na Kabi kupitia ujumbe alioupakia kwenye ukurasa wake wa instagram ni kwamba anaharibu familia yake

Baada ya mchekeshaji Flaqo kurudi mitandaoni, akiwa amejaza baadhi ya mashabiki walikana umbo lake mpya na kusema kwamba ni picha ambayo imechorwa, huku baadhi wakimpongeza na kuogopa kuwa wapenzi wao wanaweza mpenda sana kuwaliko.

Muunda maudhui  Kabi Wajesus ni miongoni mwa watu ambao wanaogopa wake zao wanaweza kumpenda Flaqo na kuwaacha.

Kulingana na Kabi kupitia ujumbe alioupakia kwenye ukurasa wake wa instagram ni kwamba anaharibu familia yake.

Milly pia ni miongoni mwa wanawake ambao walipendezwa na misuli yake Flaqo na hakuogopa kumwambia mume wake.

"Huyu Champez @flaqo411 anatuharibia ndoa nimeendea wife @the_urbanhair_salon akaniambia angalia photos za Flaqo 😡😡😡 sasa nimejaribu workout nahaiwork," Aliandika Kabi.

Pia kuna baadhi ya mashabiki wake ambao walimuonea huruma na kukiri kwamba wamepitia papo hapo, kwani wanawake wao wamekuwa wakitamani na kuwapenda wanaume wenye mwili mnene na misuli.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved