logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Mimi ni bidhaa zilizoharibika" Akothee azungumzia madhara ambayo umaarufu umemletea

Akothee amesema kuwa ingawa huwa anaonekana kuwa mwanamke jasiri, amewahi kushuhudia mengi ambayo yamevunja moyo wake

image
na Radio Jambo

Habari23 September 2021 - 07:51

Muhtasari


•Mama huyo wa watoto watano amesema kwamba anaogopa sana kukutana na watu hadharani na anatumai sana angekuwa mtu wa kawaida tu sio msanii mashuhuri.

•Akothee amesema kwamba mara nyingi amejipata akitorokea mashabiki wanaomkujia na nia ya kumsalimia kwa kuwa hapo awali amekutana na wengi ambao walijifanya kuwa nia njema ila wakageuka kuwa maadui wakubwa.

•Msanii huyo amewaomba mashabiki wake msamaha matendo yake na kudai kuwa hata yeye hayapendi na anatia juhudi kurekebisha

Mwanamuziki na mfanyibiashara mashuhuri Esther Akoth amefunguka kuhusu wakati mgumu ambao anapitia akiwa hadharani kutokana na umaarufu wake,

Mama huyo wa watoto watano amesema kwamba anaogopa sana kukutana na watu hadharani na anatumai sana angekuwa mtu wa kawaida tu sio msanii mashuhuri.

Akothee amesema kuwa ingawa huwa anaonekana kuwa mwanamke jasiri, amewahi kushuhudia mengi ambayo yamevunja moyo wake.

"Mimi ni bidhaa zilizoharibika. Nimegundua kwamba nimekuwa mtu anayewezwa na hisia sana hata sitaki tena kutoka nje ya nyumba yangu. Sipendi watu wakinitambua hadharani na kwa wakati mwingine huwa natamani tu ningekuwa mtu wa kawaida anayepita mitaani kwa amani" Akothee aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Mwanzilishi huyo wa Akothee Safaris amesema kwamba mara nyingi amejipata akitorokea mashabiki wanaomkujia na nia ya kumsalimia kwa kuwa hapo awali amekutana na wengi ambao walijifanya kuwa nia njema ila wakageuka kuwa maadui wakubwa.

"Huwa naogopa sana nikipatana na mashabiki hadharani. Pindi ninapotambuliwa, hata bila kujua huwa nasimamisha shughuli na kutaka tu kutoroka. Si jambo la kuchekesha kwa kuwa najua labda wengine huwa na nia njema ila hata walionikujia hapo awali nilidhani wako na nia njema pia" Akothee alisema.

Mwanamuziki huyo amesema kwamba ako na mashabiki wengi wanaompenda na vile vile kuna wengi ambao hawampendi

Amekiri kuwa huwa anapatwa na wasiwasi mkubwa pindi anapotoka nyumbani kwake na kushuka kutoka kwa gari kwani hajui ambacho huenda kikatokea hadharani.

"Huwa nahisi kana kwamba tayari nimeshambuliwa hata kama hakuna mtu yeyote.Hisia hiyo imenigeuza kuwa mnyama na siku moja niliuliza mshauri wangu Bi Nyongo kama maisha yangu itawahi kuwa ya kawaida tena" Alisema Akothee.

Msanii huyo amewaomba mashabiki wake msamaha matendo yake na kudai kuwa hata yeye hayapendi na anatia juhudi kurekebisha.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved