•Mwanahabari huyo amedai kwamba hamfahamu jamaa huyo na hana uhusiano wowote naye
•Amesema kwamba amekuwa akimuonya jamaa huyo kwa muda sasa ila inaonekana kana kwamba ametia masikio yake pamba.
Msomaji wa habari katika runinga ya KBC Purity Museo ametoa ombi kwa Wakenya akitaka kusaidiwa kukomesha jamaa ambaye amepamba chumba chake na picha zake.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Museo amedai kwamba jamaa anayejiita @FreeGerman2 amekuwa akimuwinda mitandaoni licha ya juhudi nyingi za kumzuia.
Museo amesema kwamba amechoshwa na jamaa huyo kwani kila anapomzuia kutoka kwa ukurasa wake huwa anaunda akaunti zingine na kuzitumia kupakia picha zake zaidi.
"Wakenya wenzangu. Nahitaji usaidizi wa kukomesha jamaa huyu! Ako na picha zangu kwenye chumba chake na kila ninapomzuia anaunda akaunti zingine na kuni'tag' kwenye chapisho zake" Museo alisema.
Mwanahabari huyo amedai kwamba hamfahamu jamaa huyo na hana uhusiano wowote naye. Amesema kwamba amekuwa akimuonya jamaa huyo kwa muda sasa ila inaonekana kana kwamba ametia masikio yake pamba.
"Simjui mimi. Nimemuonya mara kadhaa ila haskii. Sioni likiwa jambo la kawaida" Alisema Museo.
Fellow Kenyans. I need help to stop this man! He has my photos in his room and when I block him he creates new accounts and tags me in these posts. I don’t know him. I have warned him severally in vain . I don’t find this normal. His new account is @FreeGerman2 @DCI_Kenya pic.twitter.com/jKm32Luhzh
— Purity Museo (@purity_museo) September 22, 2021
Jamaa huyo anaonekana kuwa na mapenzi makubwa kwa mwanahabari huyo kwani amejaza picha zake kwenye akaunti yake.