logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Wanasema nitakufia hospitalini nikijifungua" Vera Sidika azungumza kuhusu watu wenye nia mbaya ambao wamekuwa wakimwandama

Amedai kwamba kuna baadhi ya watu ambao hawakuridhishwa na ujauzito wake na tangu alipoufichua  wamekuwa wakiomba kila uchao msiba umpate.

image
na Radio Jambo

Burudani25 September 2021 - 05:26

Muhtasari


•Mwanadada huyo mwenye umri wa miaka 31 amesema kwamba kunao watu ambao wamewahi kujaribu kumuua ila kwa neema zake Mungu hawajaweza kufaulu.

•Amedai kwamba kuna baadhi ya watu ambao hawakuridhishwa na ujauzito wake na tangu alipoufichua  wamekuwa wakiomba kila uchao msiba umpate.

•Vera ameendelea kudai kwamba watu wale wenye roho mbaya kwa sasa wanadai atapoteza maisha yake wakati atakuwa anajifungua kuona kuwa maombi yao mabaya hayajaweza kufaulu kufikia sasa.

Mwanasoshaliti mashuhuri Vera Sidika amesema kwamba kwa miaka mingi sasa kuna watu wengi  wenye nia mbaya na maisha yake ambao wamekuwa wakimuandama.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, mwanadada huyo mwenye umri wa miaka 31 amesema kwamba kunao watu ambao wamewahi kujaribu kumuua ila kwa neema zake Mungu hawajaweza kufaulu.

"Kama ni kifo, kwa miaka mingi watu wamejaribu. Lakini bado niko hapa kwa neema zake Mungu. Sio wakati wako hadi Mungu atakapoamua ni wakati wako. Binadamu watasema, wajaribu kufanya kila kitu ili wakuangamize lakini kama sio wakati wako hakuna chochote wafanyacho kinajalisha. Mungu ako nami hata mkinitumia maovu ya aina yote kila siku bado nayaepuka" Vera alisema.

Amedai kwamba kuna baadhi ya watu ambao hawakuridhishwa na ujauzito wake na tangu alipoufichua  wamekuwa wakiomba kila uchao msiba umpate.

Mama huyo mtarajiwa amedai kuna watu ambao walisema ujauzito wake ungeharibika punde baada yake kuufichua lakini nguvu za Mola zikamsaidia kuepuka laana zao.

"Wengine hata walisema ujauzito wangu ungeharibika punde baada ya kuufichua. Eti nitapoteza mtoto wangu kama bado hajazaliwa. Mambo mengi. Kama wangekuwa na nguvu nyingi kuliko Mungu , mbona wasiyatekeleze. Sasa tuko na ujauzito wa miezi nane unusu kwa sababu ya Mungu. Kila siku anaendelea kuwatia aibu" Alisema Vera.

Vera ameendelea kudai kwamba watu wale wenye roho mbaya kwa sasa wanadai atapoteza maisha yake wakati atakuwa anajifungua kuona kuwa maombi yao mabaya hayajaweza kufaulu kufikia sasa.

Hata hivyo amedai kuwa bado ako imara kwani anaamini nguvu za Maulana zinamlinda.

"Sasa  wamehitimu wanadai eti nitafariki wakati nitakuwa najifungua mtoto wangu. Yale maovu ambayo watu wananitakia na kuniambia usoni!! Hebu tafakari mtu akichukua muda wake kuandikia mwanamke mjamzito ujumbe kama huo" Alisema.

Mwanasoshalaiti huyo amesema kwamba ujasiri wake ndio umemsaidia kubaki imara licha ya maovu ambayo watu wamekuwa wakimtakia na kumwambia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved