logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sitarajii mtoto mwingine tena, nimetosheka na watoto wawili-Asema Cate Actress

Cate hakusema wala kufichua sababu ya kusema hayo

image
na Radio Jambo

Habari05 October 2021 - 14:22

Muhtasari


  • Wengi walimfahamu kupitia katika kipindi cha Mother-In-Law, na ameendelea kutia bidii katika kazi yake huku akifahamika sana mitandaoni
Kate-Actress-looking-great

Wengi walimfahamu kupitia katika kipindi cha Mother-In-Law, na ameendelea kutia bidii katika kazi yake huku akifahamika sana mitandaoni.

Akiwa kwenye mahojiano muigizaji Cate amefichua kwamba ametosheka na wanawe wawili, na wala hatawahi zaa tena.

Licha ya kuwa na ujauzito mwema wa mwanawe wa pili, amesema kwamba hatarajii kupata mtoto mwingine.

Cate hakusema wala kufichua sababu ya kusema hayo na wala hakujali kile wanamitandao watasema kuhusu usemi wake.

"Sijaolewa kwa muda mrefu kutoa ushauri kwa wanandoa lakini inafanya kazi basi ni nzuri, ikiwa haifanyi kazi basi sidhani wewe unatakiwa kujiua ukijaribu kuifanya ifanye kazi, namaanisha usiteseke

Sidhani kuwa nina usawa, najaribu tu kufanya kile ninachoweza, lakini ni nzuri kwamba nina mshirika anayeunga mkono. Kwa hivyo sio shida kwa mimi. mimi ni mwadilifu

Nina watoto wawili na nimemaliza,"Alisema Cate.

Wakati wa mahojiano, Kate pia alisema anawekeza sana katika sanaa yake ili kuendelea kuwa muhimu katika tasnia.

"Ninajaribu iwezekanavyo kuwekeza tena mara moja kwa wakati ili niweze kuendelea na mwenendo."

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved