logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nyota wa sinema Alec Baldwin amuua mwanamke kutumia bunduki wakati wa kutengenezwa kwa filamu yake

Mwanamke alikufa na mwanaume kujeruhiwa baada ya muigizaji Alec Baldwin kufyatua risasi kutumia bunduki ya maigizo kwenye seti ya filamu huko New Mexico.

image
na Radio Jambo

Habari22 October 2021 - 07:51

Muhtasari


•Mwanamke alikufa na mwanaume kujeruhiwa baada ya muigizaji Alec Baldwin kufyatua risasi kutumia bunduki ya maigizo kwenye seti ya filamu huko New Mexico.

•Msemaji wa Bw Baldwin aliliambia shirika la habari la AP kwamba kisa hicho kilihusisha utumiaji mbaya wa bunduki ya maigizo.

Mwanamke amekufa na mwanaume amejeruhiwa baada ya muigizaji Alec Baldwin kufyatua risasi kutumia bunduki ya maigizo kwenye seti ya filamu huko New Mexico.

Polisi katika jimbo hilo la Marekani walisema Bw. Baldwin alitoa silaha hiyo wakati wa utengenezaji wa filamu yake

Mwanamke huyo alipelekwa hospitalini lakini alifariki kutokana na majeraha yake. Mwanaume aliyejeruhiwa -mkurugenzi wa filamu, alikuwa akipokea huduma ya dharura.

Msemaji wa Bw Baldwin aliliambia shirika la habari la AP kwamba kisa hicho kilihusisha utumiaji mbaya wa bunduki ya maigizo.

Mwanamke huyo ametajwa kama Halyna Hutchins, 42, ambaye alikuwa akifanya kazi kama mkurugenzi wa upigaji picha. Mtu anayetibiwa ni Joel Souza, 48, mkurugenzi wa filamu.

Polisi bado wanachunguza tukio hilo huko Bonanza Creek Ranch, eneo maarufu la utengenezaji wa sinema, na hakuna mashtaka yoyote yaliyofunguliwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved