Baba kutoka Jahanamu!Baba yangu alikuwa ananilazimisha tufanye ngono-Mwanamke asimulia

Muhtasari
  • Kulingana naye baba yake mzazi alikuwa anamlazimsha wafanye ngono naye , alipokuwa shule ya upili
black-woman-crying-
black-woman-crying-

Kuna baadhi ya watu ambao wamepitia magumu maishani mwao, hamna mwanamke ambaye anapenda kufanya ngono na baba yake mzazi.

Lakini licha ya hayo yote kuna baadhi ya wanaume ambao hawatambui tamaduni za mila, huku wakiwamezea watoto wao wasichana mate.

Nikiwa kwenye ziara zangu nilipatana na mwanamke ambaye alinisimulia hadithi yake ya kutoenda nyumbani.

Kulingana naye baba yake mzazi alikuwa anamlazimsha wafanye ngono naye , alipokuwa shule ya upili.

"Sababu yangu kuu ya kutoenda nyumbani baada ya kutoroka kwa miaka 20 sasa ni kwa sababu nilipokuwa katika shule ya upili baba yangu alikuwa ananilazimisha tufanye ngono

Kwa maana hakuwa baba yangu, bali alikuwa wa kambo mama yangu hangeweza kunitetea nilipomwambia ukweli wote.

Sasa baba yangu wa kambo ni marehemu, ila sikuhudhuria mazishi yake kwani, kumbukumbu za yale alikuwa ananifanyia zinaniandama

Ushauri wangu kwa wazazi ni kuwa wanapaswa kuwa na wakati na watoto wao hasa wa kike, na kuzingatia yale yote wanaambiwa na binti zao,singetamani mtoto yeyote wa kike kupitia yale nilipitia."