logo

NOW ON AIR

Listen in Live

MC Jessy alenga kuingia bungeni 2022

Wasanii na watu wengine mashuhuri ambao wanamezea viti vya ubunge ni pamoja na Felix Odiwour (Jalang'o)-Lang'ata, MacDonald Mariga-Kibra, Authur Mandela (Xtian Dela)- Westlands, Jackson Ngechu Makini (Prezzo)- Kibra kati ya wengine wengi.

image
na Radio Jambo

Habari10 November 2021 - 05:38

Muhtasari


•Jessy ametangaza atakuwa kwenye kinyang'anyiro cha kiti cha ubunge cha eneo la Imenti Kusini, kaunti ya Meru.

•Wasanii na watu wengine mashuhuri ambao wanamezea viti vya ubunge ni pamoja na Felix Odiwour (Jalang'o)-Lang'ata, MacDonald Mariga-Kibra, Authur Mandela (Xtian Dela)- Westlands, Jackson Ngechu Makini (Prezzo)- Kibra kati ya wengine wengi.

MC Jessy akutana na wazee kutoka South Imenti wikendi iliyopita

Huku kampeni za chaguzi za mwaka wa 2022 zikiwa zimeanza kunoga kote nchini wagombeaji wapya wa viti mbalimbali  wameendelea kujitokeza.

Wasanii na watu mashuhuri wengi wameonekana kumezea mate viti mbalimbali vya kisiasa huku wengine tayari wakiwa wametangaza azma yao.

Msanii wa hivi karibuni kutangaza kujiunga nia yake ya kuwania kiti mwaka ujao ni mchekeshaji Jasper Muthomi almaarufu kama MC Jessy.

Kupitia mitandao yake ya kijamii, Jessy ametangaza atakuwa kwenye kinyang'anyiro cha kiti cha ubunge cha eneo la Imenti Kusini, kaunti ya Meru.

Wikendi  iliyopita msanii huyo wa Churchill Show alipokea wazee kutoka eneo bunge la Imenti Kusini ambao walimpa baraka anapotazamia kuanza kampeni zake.

"Wanasema ambacho wazee wanaona  wakiwa wameketi, wanaume wadogo wataweza kuona tu wakiwa wamekantanga mabega yao. Mimi ni mwanafunzi wa theolojia na naamini kwamba darasa nzuri zaidi ni kwenye miguu ya wazee. Wikendi iliyopita nilifurahia kupokea wazee ambao walinilea na ambao wametoka kutoka eneo bunge langu South Imenti na wakanipa baraka na majukumu ya kuongoza Imenti Kusini" Jessy alisema.

Jessy anatazamia kumbandua Kathuri Murungi ambaye sasa amekalia kiti hicho kwa muhula wa pili mfulululizo.

Wasanii na watu wengine mashuhuri ambao wanamezea viti vya ubunge ni pamoja na Felix Odiwour (Jalang'o)-Lang'ata, MacDonald Mariga-Kibra, Authur Mandela (Xtian Dela)- Westlands, Jackson Ngechu Makini (Prezzo)- Kibra kati ya wengine wengi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved