logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tuwaruhusu watoto wakue katika mazingira yaliyojaa upendo-Akothee kwa wazazi

Msanii huyo alisisitiza na kusema kwamba miaka 5 ya kwanza kwa mtoto ni ya muhimu,

image
na Radio Jambo

Habari11 November 2021 - 11:52

Muhtasari


  • Akothee awasisitizia wazazi kuwalea watoto wao kwenye mazingira yaliyojaa upendo

Kwa hakika tunapozungumzia wazazi ambao wwamewalea watoto wao na heshima na kuonyesha mfano mwema mitandaoni msanii Akothee hawezi salia nyuma.

Mama huyo wa watoto 5 kupitia kwnye ukurasa wake wa instagram amewashauri wazazi kuwalea watoto wao katika mazingira yaliyojaa upendo.

Pia Akothee amesimulia jinsi alikuwa napigana na baba wa watoto wake mbele ya watoto wake, alisema haya baada ya kupakia picha ya zamani akiwa na wanawe wawili.

Msanii huyo alisisitiza na kusema kwamba miaka 5 ya kwanza kwa mtoto ni ya muhimu, kwani hujenga tabia yake.

"Miaka 5 ya kwanza ya mtoto ni muhimu sana katika kujenga tabia, ni miaka 5 ya kwanza ambayo itaamua mustakabali wa tabia za watoto wako

Inasikitisha sana kuona wazazi wakiwanyima watoto wao fursa ya kuunganishwa na kujua baba/mama yao ni nani

Kusimulia watoto hadithi zisizo sahihi kuwapa watoto mtazamo mbaya na mbaya kuhusu mzazi wao mwingine.

Ni makosa, ni Mbaya sana. Tuwaruhusu watoto wakue katika mazingira yaliyojaa upendo na kukubalika

Nakumbuka nilipokuwa siwezi kumwelewa baba Oyoo na wazimu wangu, nilikuwa nafanya upasuaji kutoka nje 🤣🤣🤣. Watoto wetu walipata tu kuona vurugu moja na ambayo haikua nzuri

Tangu siku hiyo, kutokubaliana OYOO angekuja na kusimama katikati @oyootheprince : baba! Mama ! Hakuna kupigana, hakuna kubishana kila mtu aondoke kwenye sakafu sasa 🤦🏻🤔. Mungu azilinde familia zako 🙏," Allishauri Akothee.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved