logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Tabia zake ni zangu,'Vera Sidika azungumzia mwanawe

Vera alifichua kuwa yeye na mumewe huwa wanamtunza kifungua mimba wao Asia.

image
na Radio Jambo

Habari12 November 2021 - 20:45

Muhtasari


  • Vera Sidika alifichua kuwa ingawa ana kijakazi, hajawahi kuruhusu mfanyikazi wake kumtunza mtoto wake
  • Vera alifichua kuwa yeye na mumewe huwa wanamtunza kifungua mimba wao Asia

Vera Sidika ni miongoni mwa watu mashuhuri ambao wanafurahia safari yao ya kuwa mama, kwa mara ya kwanza.

Vera Sidika alifichua kuwa alichagua kuwa mama wa kudumu kwani miaka michache ya kwanza ya mtoto ni muhimu sana.

Vera Sidika alifichua kuwa ingawa ana kijakazi, hajawahi kuruhusu mfanyikazi wake kumtunza mtoto wake.

Vera alifichua kuwa yeye na mumewe huwa wanamtunza kifungua mimba wao Asia.

Mtoto Asia anaonekana kuwa mtoto mwenye bahati sana. Mtoto wa Vera kwa sasa ana wafuasi zaidi ya elfu hamsini kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Hata hivyo Vera hajawahi kuweka picha zozote za bintiye mtandaoni,Vera alidai kwamba binti yake anafanana sana na baba yake kimwili.

Hata hivyo Vera amefichua kuwa tabia za bintiye ni zake 100%.

Vera amefichua jinsi hasira ya mtoto wake inavyoweza kupanda kutoka kiwango cha moja hadi 100 ndani ya sekunde

"Asia huwa anafanya nyuso za kupendeza,yangu ya kupendeza ni ile ananung'unika ni nzuri sana, sijui huwa anazitoa wapi

Pia huwa anafanya uso akiwa amekasirika kwa kukuangalia na upande wa jicho,ukicheza na maziwa yake

Kwa maana matiti saa zingine huwa inatoka akiwa anazubaa, pia ana hasira za haraka, huwa inapanda kutoa asilimia 0 hadi asilimia 100, hayo yote ni DNA yangu," Aliandika Vera.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved