logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Hata nikifa, lazima nife nikiwa mwenye raha" Akothee asema huku akiendelea kupokea matibabu hospitalini

Mama huyo wa watoto watano amelazwa katika wadi ya wagonjwa maarafu katika hospitali moja nchini.

image
na Radio Jambo

Habari15 November 2021 - 09:36

Muhtasari


•Mama huyo wa watoto watano amelazwa katika wadi ya wagonjwa maarafu katika hospitali moja nchini.

•Mwanamuziki huyo ameendelea kupokea wageni mbalimbali pale hospitalini  haswa wa familia yake

Mwanamuziki na mjasiriamali mashuhuri nchini Esther Akoth almaarufu kama Akothee angali anaendelea kupokea matibabu hospitalini ambako alilazwa mwishoni mwa wiki iliyopita kufuatia maradhi yasiyotambulishwa.

Mama huyo wa watoto watano amelazwa katika wadi ya wagonjwa maarafu katika hospitali moja nchini.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Akothee ameonyesha hali ya kifahari ya chumba alicholazwa huku akionekana akihudumiwa na wauguzi maalum.

Kando na kitanda cha wagonjwa chumbani kile pia kina kabati kubwa, meza na viti vya wageni aina ya sofa na eneo la kupikia.

"Hata kama nitakufa, lazima nife nikiwa mtu mwenye raha" Akothee ameandika kuashiria kuwa anafurahia mandhari ya wadi aliyolazwa.

Mwanamuziki huyo ameendelea kupokea wageni mbalimbali pale hospitalini  haswa wa familia yake.

Mamia ya mashabiki wake wameendelea kumtumia jumbe za kumtakia afueni ya haraka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved