logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kuwa single ni chaguo la mwanamke,mwanamume ni kitu rahisi kupata-Amber Ray asema

Kwake, kupata mwanaume wa kuchumbiana ni jambo rahisi zaidi maishani mwake.

image
na Radio Jambo

Habari15 November 2021 - 11:09

Muhtasari


  • Mwanasosholaiti Faith Makau anayejulikana zaidi kama Amber Ray ametumia ukurasa wake wa Instagram kudokeza kwamba yuko single

Mwanasosholaiti Faith Makau anayejulikana zaidi kama Amber Ray ametumia ukurasa wake wa Instagram kudokeza kwamba yuko single.

Kulingana na sosholaiti huyo, madai ya baadhi ya wanawake kwamba wameshindwa kupata mwanamume si ya kweli.

Kwake, kupata mwanaume wa kuchumbiana ni jambo rahisi zaidi maishani mwake.

Hii inaweza kueleza kwa nini Amber Ray bado hajaolewa baada ya kutengana na mfanyabiashara wa Nairobi Jimal Roho Safi miezi michache iliyopita, ndoa ambayo ilikuwa na utata, hasa mapigano yasiyoisha na mke wa Jimal, Amira.

"Sijui ni nani anayehitaji kusikia hili lakini kuwa mseja(single) ni chaguo la wanawake, hakuna kitu kama vile hawezi kupata mwanamume. Mwanaume ndio kitu rahisi kupata 🀣," Amber Ray alidai.

Ujumbe wake ulipokelewa na hisia tofauti kutoka kwa mashabiki na hizi hapa baadhi ya hisia zao;

agufaimali3: Amiraa umeskia?πŸ˜‚

ellah_daudi: Tell them goodπŸ˜‚πŸ˜

akardi._: Go get one for u. The streets ain't belong to u no more

mkasimelissa: Talk girl. They should know that it's always about choices. πŸ™Œ

kolawoleabiola12: Sure you have been approach by lot of man each day but the main point is the choice is yours dear


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logoΒ© Radio Jambo 2024. All rights reserved