logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mama yangu hakuniamini nilipomwambiakaka yangu alinibaka-Mwanamke asimulia

Lakini swali ni je waathiriwa huwa wanapata haki kweli?

image
na Radio Jambo

Habari16 November 2021 - 11:01

Muhtasari


  • Ni wazi kuwa wengi unyanyaswa kingono na watu wa karibu nao, familia,jamaa na ata rafiki wa karibu sana
  • Visa vya ubakaji na unyanyasaji wa ngono vimekuwa vikiripotiwa na kuongezeka kila kuchao nchini
black-woman-crying-

Ni wazi kuwa wengi unyanyaswa kingono na watu wa karibu nao, familia,jamaa na ata rafiki wa karibu sana.

Visa vya ubakaji na unyanyasaji wa ngono vimekuwa vikiripotiwa na kuongezeka kila kuchao nchini.

Lakini swali ni je waathiriwa huwa wanapata haki kweli?

Kupitia kwenye mitandao ya kijamii mwanamke mmoja alieleza jinsi ndugu yake mkubwa alimbaka, na mama yake kutomuamini baada ya kisa hicho.

Hii hapa hadithi yake;

"Ndugu yangu mkubwa alinibaka mara ya kwanza na kuambia mama yangu ila hakuniamini wala kutilia maneno yangu maanani

Alininyanyasa kingono kwa muda, lakini familia yangu haikuniamni wakati huo nilimwambia dada yangu ambaye alikuwa ameolewa kuhusu masaibu yangu na akanielewa

Nilipobarikiwa na kifungua mimba msichana, niliamua kuenda kumtembelea mama yangu, mtoto wangu alikuwa na miaka 7, ndugu yangu ule tu alinibaka, nilimpata akitaka kujaribu kumbaka mtoto wangu

Mungu naye ni nani nilimgonga na mti kwa kichwa, tuliporudi nyumbani mama yangu hakutaka maneno hayo yaende mbele, karibu nimuue ndugu yangu, mama yangu alikuwa amekasirika na akanifukuza na mtoto wangu." Alisimulia mwanamke huyo.

Je umewahi pitia kisa kama hicho na ulichukua hatua gani?

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved