logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mchekeshaji Eric Omondi aachiliwa huru, baada ya kukamatwa mapema siku ya Jumanne

OCPD wa kituo cha Central Adamson Bungei alisema Omondi alikamatwa kwa kusababisha fujo nje ya bunge.

image
na Radio Jambo

Burudani16 November 2021 - 14:52

Muhtasari


  • Mchekeshaji Eric Omondi aachiliwa huru, baada ya kumatwa mapema siku ya Jumanne

Mchekeshaji Eric Omondi ameachiliwa huru saa chache baada ya kutiwa mbaroni.

Mchekeshaji  Eric Omondi alidaiwa kuzuiliwa katika kituo cha polisi baada ya kukamatwa alipokuwa anaongoza maandamano jijini Nairobi.

Msanii huyo asiyepungukiwa na drama aliripotiwa kutiwa mbaroni asubuhi ya Jumanne alipokuwa ameongoza kikundi cha vijana kuandamana nje ya bunge la kitaifa kurekebisha sekta ya muziki nchini.

Eric alikuwa ametoa wito kwa wasanii na waandishi wa habari washirikiane naye katika maandamano kuelekea bungeni kudai kuchezwa zaidi kwa sanaa ya Kenya na malipo bora kwa wasanii wakati wa tamasha.

Mchekeshaji huyo ambaye amekuwa akivuma sana hivi karibuni anadai vituo vya burudani vicheze asilimia 75 ya muziki wa Kenya.

Baada ya mchekeshaji huyo kutiwa mbaroni hisia tofauti ziliztolewa na wanamitandao, huku msanii KRG akidai kwamba Eric hapaswi kutiwa mbaroni, kwani anapigania haki za wasanii.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instaram KRG aliwafahamisga mashabiki wake kwamba mchekeshaji huyo ameachiliwa.

OCPD wa kituo cha Central Adamson Bungei alisema Omondi alikamatwa kwa kusababisha fujo nje ya bunge.

"Hakuwa amefuata taratibu za kufanya maandamano. Hata hivyo tunampanga,” Bungei alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved