Mke wangu aliniacha miezi 4 baada ya harusi yetu na kuolewa na ex wake-Jamaa asimulia

Kuwa muangalifu kuhusu  mtu unayemuahidi ndoa .Kuna watu ambao wanaingia katika maisha yako wakiwa na  nia tofauti na watu wengi watakupa  visa vya jinsi walivyokuwa waathiriwa .

Lakini kuna uchungu  ambao hauwezi kutulizwa kwa mtu kusema pole . Uchungu  wa aina hiyo ni kama anaopitia  Jared .

Baada ya uhusiano wa kimapenzi uliodumu kwa miaka mitatu na hatima yake ikaonekana kuwa ndoa ya kudumu maishani ,Jared hakuwa na shaka kwamba mke wake atakuwa  Stacy milele .

Iwapo ungemuambia kwamba miaka miwili ijayo hawangekua pamoja basi papo hapo angekuita adui mkubwa wa maendeleo yake .

Unaweza kufikiri  kwamba unamjua mtu hadi wakati anapofanya jambo fulani kisha unagundua kwamba my friend  humjui kabisa .

 Can You imagine   baada ya  Jaredkumuoa Stacy katika harusi ya kifahari ,ghafla  mpenzi wake alianza kubadilika tabia na kufanya vitu ambavyo havikueleweka .

Pindi Stacy alianza kupata shughuli ambazo hazikuwa katika mipango .mawasiliano  kati yao pia yalianza kukatika na  maneno matamu yaliokuwa ya kawaida kama vile  I miss you  na I love you yalianza kuwa nadra sana kutoka  katika kinywa chake . 

Jared aligundua kuna tatizo  na kweli hisia zake hazikumsaliti .

Yamkini ilikuwa bayana kwamba Stacy alikuwa  keshatekwa fikra na mtu  mwingine lakini  Jared alishangaa mbona basi asiseme wazi ili waachane rasmi .

Kumbe makubwa yalikuwa njiani yamemgonja Jared ! Stacy alikuwa kapendana naex wake wa kitambo  Msichana  bila aibu aliamka siku moja na kumuambia Jared kwamba ‘ You are not mature enough for me,but my ex is’ .

Kwake Jared ,yote haya yalikuwa kama ndoto lakini kwa kweli ndio ulikuwa mwanzo wa ngoma .

Hakuelewa ni vipi msichana ambaye wamekuwa naye katika uhusiano  kwa muda huo  mrefu  na hata kufunga pingu za maisha naye anavyoweza kusema kwamba yuamtaka ex wake.

"Miezi minne baadaye aliniacha na kumrudia ex wake, nadhani alikuwa amenipenda kwa ajili ya pesa zangu

Kwa kweli sikuelewa jinsi alivyoniacha ata baada ya kupitia mengi naye."